• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Government Communication
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

ZAIDI YA AJIRA 100,000 KUZALISHWA WILAYANI KILWA KUTOKANA NA MRADI WA MIHOGO

Posted on: November 29th, 2025

ZAIDI YA AJIRA 100,000 KUZALISHWA WILAYANI KILWA KUTOKANA NA MRADI WA MIHOGO 

Siku moja baada ya kutangaza mikakati nane (8) inayolenga kukuza uwekezaji nchini, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Novemba 29, 2025 amemkabidhi Mwekezaji Pan Tanzania Agriculture Development eneo la mradi lililopo Kilwa, Mkoani Lindi. 

Prof. Mkumbo amemkabidhi mwekezaji huyo eneo lenye ukubwa wa hekari 62,000 ambapo atatekeleza mradi wa kilimo cha mihogo, ujenzi wa viwanda vya uchakataji, na kuzalisha Unga kwa lengo la kuuza nje. 

Akikabidhi mradi huo, Mhe. Prof. Mkumbo amesema kuwa mradi huo unakidhi vigezo vitano vya kuchagua sekta za kimageuzi, ambavyo pia ni vigezo vya kuchagua aina ya uwekezaji utakaopewa kipaumbele kama vinavyopendekeza Dira 2050. 

Alitaja vigezo hivyo kuwa ni: 

1. Uwezo wa mradi kuzalisha ajira: Mradi unazalisha zaidi ya ajira 100,000. 

2. Uwezo wa mradi kuongeza mapato ya nje: Utachakata mihogo na kuuza unga nje ya nchi. 

3. Uwezo wa mradi kuongeza thamani: Mwekezaji atalima na kuchakata, akiongeza thamani ya zao. 4. Kigezo cha kuleta ujuzi: Mradi unatarajiwa kuwajengea uwezo wakulima wa zao la mihogo zaidi ya 10,000. 

5. Uwezo wa mradi kuchagiza sekta nyingine: Unategemea kujenga viwanda vya kuchakata bidhaa na kuleta mtaji wa nje unaokadiliwa kufikia Dola za Marekni bilioni 640. 

Awali, Mkurugenzi wa Idara ya Uwekezaji Sekta Binafsi, Bw. Aristides Mbwasi, alitoa salamu za Katibu Mkuu, Dkt. Tausi M. Kida, amesema kuwa makabidhiano hayo yanaashiria hatua muhimu katika safari ya Tanzania ya kubadilisha kilimo kuwa sekta ya kisasa, yenye ushindani, na inayoendeshwa na uwekezaji.

"Mkataba huu wa Maendeleo ya Ardhi unawakilisha utayari wetu wa kushirikiana na washirika wa kimkakati ambao huleta teknolojia, mtaji, na utaalamu ambao utainua jamii za wenyeji," amesema Bw. Mbwasi.





Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • KIKAO KAZI CHA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII MKOA WA LINDI

    December 02, 2025
  • "SHINDA VIKWAZO IMARISHA MWITIKIO, TOKOMEZA UKIMWI."

    December 01, 2025
  • ZAIDI YA AJIRA 100,000 KUZALISHWA WILAYANI KILWA KUTOKANA NA MRADI WA MIHOGO

    November 29, 2025
  • UJENZI WA BANDARI KILWA WAFIKIA 87.3%

    November 28, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.