• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

IDARA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI

BIASHARA NA UWEKEZAJI

1.0       Hali ya biashara

Biashara katika Mkoa inakua kwa kasi ya wastani kwani shughuli muhimu za kiuchumi Mkoani ni za kilimo pamoja na Uvuvi. Serikali imerejesha utaratibu wa kutoa leseni za biashara kwa kutoza ada kama ilivyokuwa mwaka 2004 na hivyo kuziwezesha Halmashauri zetu kujiongezea mapato ya ndani kutokana na chanzo hiki.

2.0       Wawekezaji

Katika kuhakikisha fursa za mkoa wa Lindi zinatumika ipasavyo, mkoa unaendelea kukusanya takwimu za uwekezaji kutoka halmashauri zote za mkoa wa Lindi  ili kuweza kuwa na mikakati madhubuti ya uwekezaji na hadi sasa tuna takwimu za halmashauri mbili ikiwemo Nachingwea na Manispaa ya Lindi  ambapo takwimu hizo zinaonyesha jumla ya wawekezaji walioko Manispaa ya Lindi  ni 154 na Nachingwea ni 23, takwimu hizo zikihusisha wawekezaji wadogo na wakubwa.

3.0       Hali ya viwanda

Mkoa wa Lindi kama ilivyo kwa mikoa mingine inavyo viwanda vya aina tatu ambavyo ni viwanda vikubwa; vya kati na vidogo. Katika mkoa tunavyo viwanda vikubwa vitatu vya kubangua korosho ambavyo kwa sasa vyote vimefungwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uchakavu wa mitambo. Aidha kwa kushirikisha wadau mbalimbali; juhudi zinafanywa ili viweze kufufuliwa na vifanye kazi ya kuongeza thamani ya zao la korosho, kuongeza ajira hatimae kuongeza thamani ya zao la korosho katika soko la ndani na nje. Mkoa pia una viwanda vya kati ambavyo kwa kiwango kikubwa vinajihusisha na uchakataji wa magogo na mbao katika wilaya zote tano za mkoa wetu. Hivi pia vimewezesha kupanua uwanda wa ajira kwa wakazi wa mkoa wa Lindi.

Vipo pia viwanda vidogo ambavyo kwa kiwango kikubwa vinachangia katika kutoa ajira na kuinua pato la kaya na jamii kwa ujumla. Viwanda hivi ni vile vya kusindika samaki (Kamba kochi na pweza) vilivyopo Kilwa, viwanda vidogo vya useremala, ukamuaji mafuta ya alizeti, ubanguaji mdogo wa korosho, ushonaji nguo hasa unifomu za wanafunzi,uchomeaji wa vyuma vya matumizi ya majumbani, karakana  na viwandani, utengenezaji wa matofali ya ujenzi wa nyumba na barabara na usindikaji wa unga wa muhogo na viwanda hivi vinapatikana katika wilaya zote za mkoa wa Lindi.

4.0       Uwekezaji Mkubwa Katika Ardhi Kwa Lengo La Kukuza Viwanda

Mkoa wa Lindi umepokea wawekezaji wengi wakubwa katika ardhi ambao uwekezaji wao una mahusiano ya karibu na ukuzaji wa viwanda. Aidha hadi kufikia mwaka 2015/2016 wawekezaji 6 wameonesha nia ya kuwekeza katika ardhi uwekezaji ambao utachangia upatikanaji wa ajira, uongezaji kipato na upunguzaji umaskini na uanzishwaji wa viwanda vya kuchakata gesi asilia, madini ya risasi, na viwanda vya mihogo kama ilivyooneshwa katika jedwali na. 1

Jedwali Na. 1: Uwekezaji Katika Ardhi Ambao Shughuli Zake Zinaendelea Kwa Sasa

Na
Kampuni Ya Uwekezaji
 Mahali Anapowekeza.
Matumizi Ya Ardhi
Ukubwa Wa Ardhi (Ha.)
Hali Halisi
1.
CASSAVA STARCH OF TANZANIA  CORPORATION LT.D
 Wilaya ya Lindi. Vijiji 6 vya Mandwanga, Linoha, Nahukahuka A na B, Lipome na Lindwandwali.
Kilimo cha Mihogo
3,004.011
Amekwishapata hekta1,752. Uthamini Kijiji Lipome, Lindwandwa
li na Linoha umekamilika.
Fidia imelipwa kijiji cha Lipome na Lindwandwali.
2.
URANEX
Wilaya ya Ruangwa. Vijiji sita 7 vya mradi wa machimbo ya Graphite.
Machimbo ya madini ya Risasi (Graphite)
3,013
Uthamini kwa ajili ya fidia umekamilika na ulipaji wa fidia unaendelea unatarajia kukamilika mwezi huu wa Januari, 2017.
3
TPDC/ MINJIGU PHOSPHATE MINING
Wilaya ya Kilwa. Eneo la katika Kiwanja Na. 1 Kitalu K. KILAMCO Kilwa Mjini.
Ujenzi wa Kiwanda cha Mbolea
60
Usanifu mradi na Uthamini wa mali katika eneo hilo umekamilika.
4
M/S OYO REAL ESTATE CO. LTD
Wilaya ya Kilwa. Vijiji vya Mtandi na Rushungi.
Viwanda vya mazao ya mafuta.
1,426.
Mpango wa Matumizi ya Ardhi na uhawilishaji umekamilika
5
GREEN RESOURCES TZ. LTD.
Wilaya ya Lindi. Vijiji vya vine (4) Hingawali, Msangya- Navanga, Nachunyu, Simana n.k
Kilimo cha Miti ya mbao na utunzaji mazingira
2,500
Mpango wa Matumizi bora uko Wizara ya Ardhi kuidhinishwa.
6
STAT OIL, EXONMOBIL, OPHIR ENERGY, SHELL LTD & PAVILION, Ophir
Manispaa ya Lindi. Eneo la Kikwetu.
Ujenzi wa Mtambo wa Gesi Asilia (LNG)
 2,071
Upimaji ardhi na Hatimiliki umekamilika. Uthamini umekamilika.
Fidia bado.

 

5.0       Mikakati iliyowekwa kimkoa

Kutokana na mkoa wa Lindi kuwa na fursa nyingi za uwekezaji, bado mkoa unahitaji kuwa na  wawekezaji wakubwa watakaoweza kuzitumia fursa hizo ipasavyo. Mikakati madhubuti ya kutangaza utajiri wa fursa za mkoa wa Lindi kwa wawekezaji wakubwa zimewekwa na zimeanza kufanyiwa kazi ya utekelezaji. mikakati hiyo ni kama ifuatayo;

  1. Mkoa kuandaa kongamano kubwa la uwekezaji “INVESTIMENT FORUM” litakalowahusisha viongozi mashuhuri wa kitaifa na wafanyabiashara wakubwa wa ndani na nje, wakiwemo mabalozi wa nchi mbalimbali. Aidha  kongamano hilo litatumika kutangaza fursa zote za uwekezaji zinazopatikana mkoa wa Lindi ikiwemo uwekezaji katika kilimo cha korosho, ufuta na mazao mengine kutokana na ukubwa wa eneo la mkoa wa Lindi. 
  2. Mkoa kushirikisha taasisi za kijamii na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali katika kufanya kampeni ya mabadiliko ya tabia ya kupuuzia kilimo na kazi za kilimo kwa jamii ya Lindi  iwe kipaumbele na  kwenda sawa na kauli mbiu ya serikali ya awamu ya tano ya “HAPA KAZI TU”
  3. Mkoa kufuatilia maazimio ya kutenga maeneo kwa ajili ya kilimo cha kisasa kwa wananchi na wawekezaji wan je na ndani katika kila Halmashauri.

5.1       Utengaji wa maeneo kwa ajili ya wafanya biashara ndogo ndogo (Machinga)

Mkoa katika kutekeleza agizo la Waziri Mkuu kuhusu kutenga maeneo ya wafanya biashara ndogo ndogo, tayari maeneo hayo yametengwa kama inavyooneshwa katika Jedwali Na. 66

Jedwali Na. 2 Maeneo Yaliyotengwa Kwa  Ajili  Ya Biashara Ndogo Ndogo Katika Mkoa wa Lindi

Na
Halmashauri
Maeneo
Maelezo
1
Lindi Manispaa
Mwenge Saba saba Mitwero
Ukubwa wa maeneo yaliyotengwa ni ekari zisizopungua 5
2
Lindi
Mihogoni-Mtama
Tayari viwanja 350 vimetengwa kwa ajili ya wafanyabiashara ndogo ndogo
3
Kilwa
Kilwa masoko
Ukubwa wa maeneo yaliyotengwa ni Ekari 6.37
4
Nachingwea
Block F (VODA)
Eneo lenye uwezo wa wafanyabiashara 150
Uhindini Block C
Eneo lenye uwezo wa wafanyabiashara 80
Bondeni area
Eneo lenye uwezo wa wafanyabiashara 300
5
Ruangwa
Kilimahewa, Dodoma na Namakonde
Ukubwa wa maeneo yaliyotengwa ni ekari zisizopungua 5
6
Liwale
Eneo la wajasiliamali vijana na wanawake liwale
Ukubwa wa maeneo yaliyotengwa ni ekari zisizopungua 4
Eneo la soko
Ukubwa wa maeneo yaliyotengwa ni ekari zisizopungua 1
Eneo la viwanda vidogo (SIDO)
Ukubwa wa maeneo yaliyotengwa ni ekari zisizopungua 1


MAENEO NA FURSA KWA AJILI YA UWEKEZAJI KWA KILA HALMASHAURI KATIKA MKOA WA LINDI

Na. 
Halmashauri 
Eneo Liliotengwa 
Ukubwa wa eneo (Ha) 
Matumizi 
Maelezo 
1
Lindi MC
Mkwaya-Likono
Km 112
Fukwe kwa ajili ya burudani
Eneo la pembezoni mwa bahari ya Lindi
Kikwetu
2,071.705
LNG
limeshapimwa

5,000
Chuo Kikuu
Limetengwa halihitaji fidia
2
Lindi DC
Mipingo
322,705
Kilimo cha Ufuta
Eneo limetengwa, Halijapimwa
Chiponda
48,908
Ufugaji wa nyuki katika misitu
Eneo halijapimwa lakini halihitaji fidia
Sudi, Mchinga, Mongomongo, Shuka, Ruvu
Km 170
Hoteli na maeneo ya burudani
Halijapimwa, linahitaji fidia
3
Kilwa
Matandu, Bonde la Mavuji, Migurue na Lihimalyao
47,223
Kilimo
Eneo lina milikiwa na kijiji halijapimwa
Hoteli tatu, Kivinje na Kilwa Masoko
500
Viwanda
Eneo lina milikiwa na kijiji halijapimwa
Kilwa Kisiwani, Kilwa kivinje, Nang’oma na Selous
844.24
Utalii
Eneo limetengwa lakini halijapimwa
Kisiwa cha Songosongo, Kilwa Kivinje, Somanga, Kilwa Kisiwani, na Songomnara
1,221.52
Uvuvi
Eneo limetengwa lakini halijapimwa
Mandawa, Hoteli tatu na Mavuji
200
Madini
Eneo limetengwa lakini halijapimwa
4
Ruangwa
Luchelegwa, Mnacho na Makanjiro
127,999
Kilimo cha Mihogo na ufuta
Limepimwa na linahitaji fidia
Kilimahewa
69
Uwekezaji wa Majengo
Limepimwa na linahitaji fidia
 5
Nachingwea
Bondeni Road
8,100
Viwanda
Limepimwa na linahitaji fidia
Bondeni Road
6,199.3
Majengo ya biashara
1,815.8Ha yamepimwa na yanahitaji fidia na yanayoendelea na upimaji 4383.5Ha
Bondeni road
8,348.1
Ujenzi wa shule
limepimwa na linahitaji fidia
 6
Liwale
Mpirani
2.4
Viwanda vya kuchakata madini,
Limepimwa, linahitaji fidia
Kichonda, Darajani na Mihumo
5,387
Kilimo cha Muhogo
Limepimwa linahitaji fidia
Jumuiya ya Magingo (WMA)
5,700
Utalii/uwindaji
Eneo lipo na linatumika kwa makubaliano na Jumuiya
Msitu wa Angai
139,420
Uvunaji wa mbao na asali
Makubaliano na vijiji kwa ajili ya uvunaji




Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.