• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Uvuvi

SEKTA YA UVUVI KWA MKOA WA LINDI.

1. Utangulizi.

Sekta ya uvuvi kwa Mkoa wa Lindi inajumuisha shughuli za uvuvi wa samaki katika vyanzo vya maji vya asili (bahari, mito, na mabwawa), shughuli ya ufugaji wa samaki na kilimo cha mwani. Kwa upande wa vyanzo vya asili Mkoa umepitiwa na Bahari ya Hindi, Mto Lukuledi, Ziwa dogo la Rutamba na Mabwawa.

2. Shughuli ya uvuvi wa samaki.

Mkoa wa Lindi una mwambao wa bahari usiopungua urefu wa km 285 kutoka Kijiji cha Sudi (Kusini mwa Wilaya ya Lindi) mpaka Kijiji cha Marendego (Kaskazini mwa Wilaya ya Kilwa). Ukanda huu wa Bahari una fukwe nyingi zinazofaa kwa ukuzaji wa viumbe vya majini kama vile samaki, kaa, chaza na kilimo cha Mwani.

Ukanda huu ndio wenye jamii inayojishughulisha na uvuvi wa samaki kwa kiasi kikubwa kutokana na uwepo wa bahari ambapo unaojumuisha Wilaya za Lindi na Kilwa. Uvuaji samaki hufanywa kwa kutumia zana na teknolojia mbalimbali (kama madema, wando, zurumati, mishipi ya mkononi, nyavu ndogo za jarife, nyavu za kilindini za kuzungusha makundi ya samaki, vimia na nyavu za dagaa) kulingana na aina tofauti za samaki wanaoruhusiwa kuvuliwa kwa mujibu wa sheria ya Uvuvi namba 22 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2009, sera ya uvuvi na miongozo mbalimbali.

Vyombo vinavyotumika kuvulia ni mashua, madau, ngalawa na mitumbwi (dugout cones) vinavyoendeshwa ama kwa kutumia matanga (upepo) au makasia.

Baadhi ya aina ya samaki wanaopatikana

  

Shughuli za usimamizi raslimali za uvuvi.

Shughuli ya usimamizi na udhibiti uvunaji raslimali za bahari unafanywa na vyombo mbalimbali vya serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Halmashauri za Wilaya zote tatu zinawajibika katika kuhifadhi na kusimamia uvunaji endelevu wa raslimali za uvuvi. Pia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kupitia vituo vyake vya doria vilivyoko Wilaya ya Kilwa na Wadau mbalimbali kama WWF wanashirikiana na Mkoa katika usimamizi wa rasilimali hizi.

Halmashauri zimeunda na zinaendelea kuunda vikundi shirikishi vya usimamizi raslimali uvuvi (Beach Management Unit, BMUs) katika vijiji na mataa ya jamii ya uvuvi.

3. Ufugaji wa samaki.

Hii ni shughuli inayofanyika katika maeneo mbalimbali ya Mkoa ambayo yana vyanzo vizuri vya maji baridi na maji chumvi. Wilaya za Ruangwa, Nachingwea na Liwale shughuli za ufugaji wa samaki zinafanyika katika vyanzo vya maji baridi na aina ya samaki wanaofugwa ni perege na kambale.

Zaidi ya hekta 10 kwa Mkoa wa Lindi zinafaa kwa kilimo cha umwagiliaji kutokana na uwepo wa mabonde ya maji yanayotiririsha maji mwaka mzima. Hivyo maeneo hayo ni fursa pia kwa ufugaji wa samaki wa maji baridi ambapo shughuli hiyo inaweza kufanywa kwa pamoja na kilimo.

Halmashauri ya Wilaya ya Lindi, Manispaa ya Lindi na Kilwa ufugaji wa samaki unafanyika katika pwani ya bahari na maeneo ya vyanzo vya maji baridi. Aina ya samaki wanaofugwa katika maeneo ni kambale, mwatiko, perege na kaa.

4. Kilimo cha mwani.

Mwani ni mimea inayoota kwenye maji, na mingine huota na kuishi katika maji chumvi na mingine katika maji baridi (mito, maziwa nk). Mfano mimea ya nchi kavu ina mizizi kwa ajili ya kufyonzea maji na chumvi ardhini, ina mashina na pia ina majani, lakini mimea aina ya mwani haina mizizi, majani wala shina, hivyo ufyonzaji wa chakula hufanywa na sehemu zote za mmea mzima.

Aina za mwani. 

  • Mwani mwekundu (Spinosum)
  • Mwani wa kijani (Cotonii)

Kwa Mkoa wa Lindi hii ni shughuli ya kilimo inayafanywa na jamii ya pwani ya bahari ambapo shughuli hiyo hufanyika ndani ya bahari.

Uwepo wa bahari Mkoani Lindi ni fursa pekee kwa wakazi wa mwambao wa pwani katika kukuza na kuendeleza kilimo cha mwani na kuweza kujiongeza kipato. Kama ilivyo shughuli ya uvuvi, kilimo cha mwani kinafanyika katika Halmashauri za Wilaya ya Kilwa, Lindi na Manispaa ya Lindi huku aina mbili za mwani cotonii na syprosum zikiwa zinalimwa kwa wingi.

Pamoja na uwepo wa bahari katika Mkoa wa Lindi uzalishaji wa zao la mwani umekuwa ukishuka kila mwaka kutokana na sababu mbalimbali hasa kushuka kwa bei ya zao hilo sokoni na magonjwa yanayoshambulia zao hilo.

Mkoa unaendelea kuhamasisha wakulima wa mwani kuuchakata mwani kwa lengo la kuuongezea thamani pamoja na kuzalisha bidhaa mbalimbali zinazotokana na mwani. Pia Mkoa kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Rasilimali Uvuvi ya TAFIRI unaendelea na tafiti mbalimbali zikiwemo za magonjwa yanayolikabili zao la mwani.

5. CHANGAMOTO NA MIKAKATI YA KUKABILIANA NAZO.

5.a. Changamoto

Pamoja na mafanikio mengi yaliyopatikana, Mkoa unakabiliwa na changamoto zifuatazo kupitia Sekta ya uvuvi:-

  • Kutokuwepo kwa Boti imara za kufanyia doria pamoja na kikosi maalum cha doria Mkoani, kwani mara nyingi kikosi kinachotumika hutokea Dar es Salaam au Mtwara na hufanya kazi kwa muda kisha huondoka. Pia upungufu wa rasilimali fedha kwa ajili ya kugharamia doria.
  • Matumizi ya zana duni za uvuvi kunasababisha pato la mvuvi kuendelea kuwa dogo,
  • Matumizi yasiyo sahihi ya malighafi za kutengeneza zana za uvuvi, mfano mshipi wa plastiki (monofilament) kutumika kutengeneza nyavu ambazo ni hatari kwa uhifadhi wa Mazingira ya Bahari.
  • Ukosefu wa maduka ya vifaa bora vya uvuvi.
  • Ukosefu wa vyama vya kuweka na kukopa (SACCOS) vya wavuvi
  • Huduma za ugani na ushauri kuwa finyu kutokana na uhaba wa watumishi na vitendea kazi (Halmashauri za Ruangwa na Liwale hazina kabisa watumishi ingawa kuna mahitaji makubwa kwa wananchi wa maeneo hayo).
  • Mabwawa mengi ya kufugia samaki kuwa mbali na makazi hivyo kuwa vigumu kwa mmiliki kuyatunza ipasavyo na kuimarisha ulinzi.
  • Gharama kubwa za upatikanaji na uandaaji wa chakula cha ziada cha samaki.
  • Ukataji wa mikoko na uharibifu wa mazingira inapelekea vyanzo vya mazalia ya samaki kuendelea kuharibika.
  • Fikra potofu za baadhi ya wafugaji wa samaki kuwa kila kitu kinatakiwa kufanywa na Serikali ama Tasisi (fikra tegemezi).
  • Tatizo la ukame na mabadiliko ya hali ya Hewa kupelekea shughuli za ufugaji wa samaki kurudi nyuma (Wilaya za Nachingwea, Liwale na Ruangwa).
  • Kutopatikana kwa urahisi mbegu bora/vifaranga vya samaki.
  • Utoaji wa pembejeo kwa ajili ya kilimo cha Mwani kunakofanywa na wanunuzi wa Mwani kwa wakulima kuna haribu zana ya soko huria na kumdhalilisha mkulima kwa kumjengea tabia tegemezi.
  • Tatizo la wanunuzi/Makampuni yanayonunua mazao ya uvuvi hasa zao la Mwani kuficha takwimu halisi za manunuzi kwa mamlaka husika kunapelekea kutokwa na usahihi wa takwimu na maendeleo kwenye zao hilo.

 5.b. Mikakati 

Ili kufikia malengo yaliowekwa katika kuendeleza sekta ya uvuvi kwa ujumla na kutokana na hali halisi ya sekta ya Uvuvi katika Mkoa wetu ukilinganisha na changamoto zilizopo kwenye Halmashauri zetu, Mamlaka za Serikali za Mitaa (MSM) hazina budi kusimamia na kuendeleza rasilimali za Uvuvi kwa kuzingatia mambo yafuatayo: -

  • MSM zitambue kuwa jukumu la usimamizi wa rasilimali za uvuvi ni la Halmashauri husika kwa mujibu wa sheria ya kuanzishwa kwake, hivyo taasisi, chombo, kikundi au mtu yeyote yule anayejishughulisha na shughuli za utunzaji, Usimamizi na uendelezaji rasilimali hizo anasaidia tu. Hivyo, kila Halmashauri itengenze mfumo utakaowaashirikisha wadau wote wa sekta ya uvuvi katika usimamizi na uvunaji wa rasilimali za uvuvi.
  • Kila Wilaya iandae na isimamie kupitia kamati zake za Ulinzi na Usalama mkakati wa kuondoa kabisa uvuvi haramu katika maeneo yao, ikiwa ni pamoja na kuwatambua wananchi wote wanaojishughulisha na Uvuvi haramu na kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria.
  • Ili kuwa na mwelekeo sahihi na kurahisisha ufuatiliaji, kila Halmashauri iandae mpango mkakati wa sekta ya uvuvi na kuainisha vipaumbele na maeneo ya kimkakati ambayo Halmashauri inajipanga kusimamia.
  • Mamlaka za Serikali za Mitaa ziweke makadirio sahihi ya mapato yatokanayo na Uvuvi. Pia zitenge fedha katika bajeti ya maendeleo kwa ajili ya kuedeleza sekta ya uvuvi katika maendeo yao. Aidha, kila Halmahsuri itenge walau 15% ya mapato yatokanayo na uvuvi kwa ajili ya kuendeleza sekta ya uvuvi.
  • Wakurugenzi wa Halmashauri wahakikishe wana wawezesha wataalamu wa sekta ya uvuvi ili waweze kuzunguka kutoa elimu, ushauri, na kusimamia shughuli za sekta ya uvuvi katika maeneo yao.
  • Wilaya na Halmashauri zifanye mafunzo au semina kwa viongozi mbalimbali (wakiwemo viongozi wa dini, siasa, wakuu wa taasisi za umma na binafsi n.k) katika maeneo yao kwa lengo la kuwajengea uelewa wa pamoja kuhusu sheria za uvuvi na mambo mbalimbali ya ujumla yanayohusu sekta ya uvuvi. Hii ni pamoja na kuwa na mikakati ya pamoja ya uendelezaji na usimamizi wa rasilimali za sekta ya uvuvi katika Wilaya na Halmashauri husika.
  •  Kila Halmashauri itunge na kusimamia sheria ndogo za kutunza na kusimamia rasilimali za uvuvi na zitakazohakikisha kuwa wataalamu na watendaji wote wanakuwa na UTAIFA, UZALENDO, UWAJIBIKAJI na wanazingatia MAADILI ikiwa ni pamoja na kulinda na kuheshimu TAALUMA.
  • Halmashauri ziviwezesha na kuvifuatilia vikundi vya usimamizi shirikishi wa rasilimali za uvuvi na kuhakikisha juhudi za pamoja zinafanyika ili kupata rasilimali fedha za kutosha kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya uvuvi, hili liende sambamba na kuangalia uwezekano wa: -

            Kurudisha asilimia (15%) kutoka kwenye makusanyo ya ndani kupitia sekta ya uvuvi ili ziweze kusaidia kuendeleza sekta.

            Kuona uwezekano wa kuvipatia vikundi vya Usimamizi wa rasilimali za uvuvi uwakala wa kukusanya mapato ili viweze kuwa endelevu.

            Kuandika maandiko ya kuomba fedha kutoka vyanzo mbalimbali na kubuni mbinu nyingine zinazoweza kuongeza rasilimali fedha kwa ajili ya kuendeleza sekta ya uvuvi.

  • Kutokana na tatizo la upungufu wa watumishi, Halmashauri za Ruangwa na Liwale.
  •  Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi iangalie uwezekano wa kuupatia Mkoa wa Lindi boti ya kisasa kwa ajili ya kufanyia doria ya kudhibiti uvuvi haramu katika pwani ya Halmashauri zote za Kilwa, Lindi na Manispaa ya Lindi.
  • Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi iangalie uwezekano wa kuanzisha kituo cha kuzalisha mbegu bora ya samaki (fingerlings) aina ya mwatiko (Milkfish) katika maeneo ya pwani kandokando mwa Bahari. Pia ikiendeleze kituo cha uzalishaji wa mbegu bora za samaki cha mtama kwa kukifanyia ukarabati ili kiweze kutoa huduma za uzalishaji vifaranga vya samaki.
  • Aidha, Halmashauri zione uwezekano wa kuanzisha mashamba darasa (mabwawa ya mfano) katika maeneo yao ili kuhamasisha wananchi katika suala la ufugaji samaki kupitia mabwawa.
  • Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi iendelee kutoa chakula cha ruzuku kwa wafugaji wa samaki.


Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.