• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Bi. Madenge: Simamieni haki za binadamu

Posted on: July 8th, 2019

Bi. Madenge: Simamieni haki za binadamu.

Watendaji wa kata wilaya ya Lindi wametakiwa kusimamia haki za binadamu na upatikanaji haki kisheria.

Hayo yamesemwa na Bi. Rehema Madenge, Katibu Tawala Mkoa wa Lindi wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa watendaji wa kata kuhusu haki za binadamu na upatikanaji haki kisheria yaliyofanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Lindi.

Bi. Madenge amesema watendaji wanao wajibu mkubwa wa kusimamia haki na upatikanaji haki kisheria. Hii ni pamoja na usimamizi wa haki za watoto ambapo kwa mkoa wa Lindi kumekuwa na tatizo kubwa la mimba za utotoni kunakopelekea watoto hao kukosa haki zao za msingi.

“Katika mkoa wa Lindi tuna tatizo kubwa la mimba za utotoni hivyo ni lazima mtambue kuwa jambo hili linasababisha watoto kukosa haki zao ikiwa ni pamoja na haki ya elimu. Hivyo ni matarajio yangu kuwa mtakapo toka hapa mtakwenda kupambana na mimba za utotoni kwa kuhakikisha wahusika wote wanachukuliwa hatua stahiki”, alisema Bi. Madenge.

Vilevile kuna makundi mbalimbali ambayo hushindwa kupata haki au kudai haki kisheria hasa ya walemavu kuanzia kwenye ngazi ya familia. Hivyo watendaji wametakiwa kwenda kutoa elimu hii kwenye maeneo wanayotoka ikiwa ni pamoja na matumizi ya madawati ya kijinsia yanayoratibiwa na polisi.

Pia Madenge amewataka watendaji hao kutumia mafunzo hayo kubadilishana uzoefu kwa kuzungumza mambo yanayowakwamisha kiutendaji na kujadili namna ya kuboresha.

Aidha, Bi Madenge amewashukuru Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, chini ya ufadhili wa Legal Service Facility (LSF) kwa kuandaa mafunzo haya ambayo yataleta tija kubwa katika kuboresha utendaji na hatimaye kuimarisha utoaji huduma kwa wananchi.

Akizungumza kabla ya ufunguzi Alexander S. Hassan, Mkurugenzi Elimu kwa Umma na Mafunzo Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora amesema mafunzo hayo ni mwendelezo wa mafunzo ambayo yalifanyika tarehe 7-11 January, 2019 yaliyowahusisha baadhi ya wakuu wa idara wa sekretarieti ya mkoa na halmashauri za mkoa wa Lindi.

Mafunzo hayo yana lengo la kuwajengea uwezo watendaji wa kata kuhusu misingi ya utawala bora na haki za binadamu ili waweze kutumia elimu watakayoipata kujitathmini katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.  

Katika mkoa wa Lindi mafunzo haya yatafanyika katika wilaya tatu za Lindi (Lindi DC na Lindi MC), wilaya ya Liwale (Liwale DC na Kilwa DC) na wilaya ya Ruangwa (Ruangwa DC na Nachingwea).

Naye Emmanuel Lweyo, Afisa Utumishi manispaa ya Lindi (Mwezeshaji) amesema mafunzo haya ni muhimu kwa watendaji kwani yapo mambo mengi ambayo yamekuwa yakifanyika kutokana na kutokuwa na uelewa kwa watendaji. Watendaji wanapaswa kuelewa mipaka yao ya kiutendaji kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu ili kuweza kutoa huduma kwa kuzingatia misingi ya utawala bora.

Issa Mbaruku, Mtendaji wa Kata ya Kitumbikwera (Mshiriki wa mafunzo) ameshukuru kupata mafunzo hayo kwani yamemsaidia sana kuhusu namna ya kupambana na ukatili wa kijinsia hasa kwa watoto wa kike. Issa amesema katika jamii hilo tatizo lipo hivyo wananchi wanatakiwa kuelimishwa zaidi juu ya namna ya upataji haki kisheria.

Pia amesema wao kama watendaji watakwenda kusimamia maagizo yaliyotolewa na Katibu Tawala Mkoa hasa katika kusimamia na kudhibiti mimba zo utotoni. Hii ni pamoja na kuwachukulia hatua wale wote watakaohusika na kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa haki za watoto.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.