• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Bi. ZUWENA OMARY ASISITIZA ELIMU ITOLEWE ZAIDI KUHUSIANA NA MPANGO WA M-MAMA

Posted on: October 10th, 2023

Katibu Tawala Mkoa wa Lindi Bi. Zuwena Omary amesisitiza kuendelea kutoa elimu zaidi juu ya mpango wa huduma ya usafiri wa dharura ujulikanao kama M-mama.

Bi. Zuwena ameyasema hayo akiwa ni mgeni rasmi katika kikao cha makabidhiano ya mpango wa M-mama kati ya serikali na wadau baada ya kukamilisha kipindi cha ushirikiano wa moja kwa moja kilichofanyika siku ya jumatatu, tarehe 09 Oktoba 2023 katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Lindi kikiwahusisha viongozi wa Mkoa, Wilaya, tamisemi, Pathfinder na Touch Foundation.

Bi. Zuwena akiwashukuru wadau waliofanikisha mpango huo ambao ni USAID, Vodafone Foundation, Pathfinder na Touch Foundation, amesema kuwa Mkoa unapoenda kutekeleza mpango wa M-mama bila wafadhili ni vyema kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika kuielimisha jamii juu ya umuhimu na matumizi sahihi ya utoaji na upatikanaji wa taarifa za wanufaika.

Ameongeza kuwa jamii ielimishwe vizuri kuhusiana na matumizi sahihi ya namba ya simu ya huduma kwa mteja ili isigeuke kuwa kero na usumbufu kwa matumizi ambayo hayatoendana na malengo husika.

" Elimu, uhamasishaji na ushirikishaji wa jamii ikiwemo viongozi wa ngazi zote ili kuhakikisha elimu kuhusu huduma ya usafiri wa dharura inatolewa kwa umma." Amesema Bi. Zuwena.

Pamoja na elimu ya mpango mzuri wa huduma ya M-mama, Bi. Zuwena amewataka wataalam wa afya kuongeza nguvu katika kutoa elimu ya chakula na lishe bora kwa mama mjamzito na mtoto ili isaidie kuondokana na changamoto ya tatizo la udumavu.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi Dkt. Kheri Kagya amesema kuwa mpango wa M-mama tangu aunze kutekelezwa Mkoani Lindi mwaka 2022 umesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto ya vifo vya mama na mtoto.

Kutokana na umuhimu na mafanikio makubwa ya mpango wa M-mama, Dkt. Kagya ameongeza kuwa Mkoa wa Lindi umejipanga vizuri kuendelea na utekelezaji wa mpango huo ambao unaenda kutekelezwa kwa asilimia 100 na Serikali.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.