• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

BILIONI 1 KUJENGA MIUNDOMBINU YA MIFUGO MKOANI LINDI

Posted on: September 23rd, 2021

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi  imetenga Jumla ya bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya mifugo mkoani Lindi.

Hayo yemesemwa  na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega alipofanya ziara ya siku nne kuanzia tarehe 20-23 Septemba 2021 ya kuwatembelea wakulima na wafugaji kwa lengo la kutatua migogoro kati ya makundi hayo mawili. Mhe. Naibu Waziri ameeleza kuwa jumla ya fedha takribani bilioni 1 zitatumika kabla ya msimu wa mvua kuanza mwaka huu 2021 katika ujenzi wa mabwawa mawili katika vijiji vya Kimambi Wilayani Liwale na Matekwe Wilayani Nachingwea, pamoja na majosho katika wilaya hizo ikiwemo na Wilaya ya Lindi.

Mhe. Naibu Waziri akizungumza na wakulima na wafugaji katika vikao vilivyofanyika vijiji vya Kimambi na Mirui Wilayani Liwale, kijiji cha Kilimarondo Wilayani Nachingwea, kijiji cha Nangulugai Wilayani Ruangwa na mtaa wa Miangala Wilayani Lindi, ameeleza kuwa miundombinu hii itatatua migogoro ya wakulima na wafugaji ambayo kwa asilimia kubwa inasababishwa na changamoto ya uhaba wa maji. Katika ujenzi wa malambo hayo, Mhe. Naibu Waziri amewataka wakandarasi pamoja na wasimamizi ngazi ya wilaya kuwashirikisha wafugaji ili mabirika ya mabwawa hayo yajengwe kwa kuzingatia mahitaji ya wafugaji hao na ikiwa kutakuwa na maboresho zaidi waombwe wafugaji na Halmashauri kuchangia gharama hizo.

Pia Mhe. Naibu Waziri amezitaka Halmashauri kuanzisha na kuboresha miundombinu ya minada ya mifugo ili kuongeza vyanzo vya mapato. Akizungumza kwenye mkutano uliofanyika kijiji cha Kilimarondo, Mhe. Naibu Waziri amewataka wafugaji wabadilike na waanze kuuza mifugo yao kwa kutumia minada iliyopo ili kuboresha maisha yao na Halmashauri kupata kipato. “ wafugaji vuneni mifugo kwa kuwauza ili mchangie pato la Halmashauri”, amesema.

Katika kikao cha majumuisho ya ziara ya Mhe. Naibu Waziri kilichofanyika tarehe 23 Septemba 2021 Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, akioneshwa kusikitishwa na migogoro ya wakulima na wafugaji Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainabu R. Telack amemweleza Mhe. Ulega kuwa licha ya mifugo kuwa chanzo cha migogoro lakini hayuko tayari kuvumilia mifugo ambayo haichangii pato lolote ndani ya Mkoa “ Mazao ya ufuta na korosho yanaingiza mabilioni ya fedha kwenye Halmashauri zetu, lakini mifugo haina mchango wowote wa mapato….kwetu sisi haina faida.” Amesema Mhe. Telack.  

Katika mikutano yake, Mhe. Naibu Waziri ameendelea kuwasisitiza wafugaji na wakulima kufanya shughuli zao kwa kuzingatia sheria za nchi, huku akiwaasa wafugaji kuwa miundombinu ya maji inajengwa na Serikali hivyo waache visingizio vya kuvamia maeneo ambayo hayakutengwa kwa ajili ya shughuli za mifugo.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.