• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Bilioni 10.4 zaboresha miundombinu ya Afya - Lindi

Posted on: February 28th, 2020

Bilioni 10.4 zaboresha miundombinu ya Afya - Lindi. 

Mkoa wa Lindi umepokea bilioni 10.4 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya na hospitali za wilaya.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM 2015-2020 katika kipindi cha Julai – Desemba, 2019 katika kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Lindi.

Mkuu wa mkoa Zambi amesema katika kuboresha huduma za afya, serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imetoa fedha za kujenga na kukarabati vituo vya afya 14, ujenzi wa hospitali za wilaya 2 (Ruangwa & Mtama) na ujenzi wa wodi ya kujifungulia 1(Nachingwea).

Katika awamu ya kwanza mkoa ulipokea Tsh. 1,500,000,000/= kwa ajili ya ujenzi wa vituo 3, awamu ya pili tulipokea Tsh. 5,100,000,000/= kwa ajili ya ujenzi wa vituo 10, na awamu ya tatu mkoa ulipokea Tsh. 3,800,000,000/= ikiwa Tsh. 400,000,000/= fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Nanjirinji, Tsh. 400,000,000/= fedha kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya wazazi na watoto katika hospitali ya wilaya ya Nachingwea, Tsh. 1,500,000,000/= kwa ajili ya ujenzi wa hospitali Wilaya - Ruangwa na Tsh. 1,500,000,000/= fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Lindi.

“Ujenzi na ukarabati huu wa vituo vya afya ni kwa ajili ya kuongeza majengo ya maabara, upasuaji, mama na watoto, jengo la kuhifadhia maiti na nyumba ya mtumishi. Kwa kufanya hivi serikali imepunguza sana tabu waliyokuwa wanapata wananchi ambao walilazimika kwenda mbali kufuata huduma hizo hasa akina mama wajawazito”, alisema Zambi.

Kwa upande wa zahanati, mkuu wa mkoa Zambi alisema kuna jumla ya zahanati 53 ambazo zinaendelea kujengwa na zipo katika hatua mbalimbali katika halmashauri zote 6 (Manispaa ya Lindi - 5, Halmashauri ya Mtama - 11, Liwale - 3, Kilwa -10, Ruangwa -11 na Nachingwea – 13). Kati ya hizo zahanati 5 zimekamilika zinasubiri kusajiliwa na serikali kuu katika bajeti 2020/2021 ili ziweze kutoa huduma. Zahanati hizo ni Faraja na Chikundi zilizopo halmashauri ya Ruangwa na Kisingo, Miumbu na Mtepera zilizopo halmashauri ya Kilwa.

Aidha, mkuu wa mkoa Zambi amesema serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya afya lengo ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora jirani na maeneo yao.

Katika kuboresha huduma za afya serikali pia imeendelea kuimarisha hali ya upatikanaji wa madawa ambapo kwa mkoa wa Lindi upatikanaji wa dawa katika vituo vyote 253 vya kutolea huduma dawa na vifaa tiba zinapatikana kwa asilimia 93.

Naye mwenyekiti wa CCM mkoa wa Lindi, Fadhili ameipongeza serikali kwa kazi kubwa inayofanyika katika kuboresha huduma za afya ambapo mkoa wa Lindi umepatiwa bilioni 10.4 kwa ajili ya kazi hiyo.

 Pia ameiomba serikali kuendelea kuboresha huduma za afya katika maeneo mengine ikiwa ni pamoja na kuongeza watumishi ili miundombinu hiyo itakapokamilika wananchi wapate huduma toka kwa wataalam. Aidha, ameishukuru serikali ya mkoa kwa ushirikiano uliopo kati ya chama na serikali.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.