• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM KUANZA UJENZI WA KITIVO CHA KILIMO MKOANI LINDI

Posted on: September 6th, 2021

Chuo Kikuu cha Dar es salaam kupitia timu ya wakufunzi chuo hicho wamewasilisha rasmi mpango wa ujenzi wa Kitivo cha Kilimo Mkaoni Lindi kwenye kikao kilichofanyika leo tarehe 06 septemba 2021 kwenye Ukumbi mdogo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi. Akiwasilisha mpango huo mbele ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Zainab Telack,  Dkt. Mkabwa L. Manoko amesema utekelezaji wa  ujenzi huo unatarajiwa kuanza mwezi huu wa Septemba 2021 eneo la Ngongo, Manispaa ya Lindi lenye ukubwa wa hekta 45.5.

Utekelezaji wa mradi huo mkubwa unakusudia kukuza muundo wa shahada ya kwanza, ubora wa programu na utoaji wa huduma unaoendana na kilimo cha mtanzania,  hii ikiwa ni lengo lililowekwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kuanzisha na kuendeleza tawi la chuo cha kilimo na teknolojia ya chakula Mkoani Lindi mpaka kufikia juni 2025.

Shughuli zilizopangwa kufanyika kwa mwaka wa fedha 2021/22 kuhusiana na ujenzi wa Kampasi ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam-Lindi (CKL) ni pamoja na ujenzi wa vyumba vya mihadhara (vyumba vya kufundishia), ofisi za wafanyakazi, maabara, bweni la wanafunzi pamoja na ununuzi wa samani, vifaa vya TEHAMA, mtambo wa kuchakata chakula, vifaa vya maabara za mazao ya kilimo , chakula na uhandisi kilimo.

Kwa mujibu wa mpango wa ujenzi huo mpaka kufikia 2027, eneo la hekta 45.5 ni dogo kutosheleza mahitaji ya Kampasi hiyo hivyo Chuo Kikuu kimeomba kipatiwe eneo lenye hekta 500 zaidi lililopo mtaa wa Nandambi ili kuweza kufanikisha huduma za chuo ikiwa pia ni fursa ya kutumia bwawa la Rutamba kwa mahitaji ya mafunzo.  Pamoja na maombi hayo ya ardhi, pia Dkt. Mkabwa alieleza kuwa ili kufikia malengo changamoto za miundombinu ya barabara, maji na umeme zinazoukabili mtaa wa Nandambi zifanyiwe kazi.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack akionesha kufurahishwa na ujio wa mradi huo wa kipekee Mkoani Lindi, amezielekeza mamlaka zote (TARURA, TANESCO Kupitia mradi wa REA) zinazohusika na mradi huo kuhakikisha miundombinu yote ambayo sio mizuri inaboreshwa na kuondoa changamoto zote zilizoelezwa. Akipokea maelekezo hayo, Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Shaibu Ndemanga amewahakikishia wakufunzi hao kuwa Wilaya ya Lindi na Manispaa yake wapo tayari kushirikiana bega kwa bega kuhakikisha huduma za maji na umeme zinapatikana eneo husika. “ Mahala ambapo kuna uwekezaji wowote hizi huduma ni wajibu wetu sisi kuzifikisha……barabara, maji, umeme na kila ambacho kinahitajika kitapatikana kwa haraka kadri itakavyowezekana.”

Uwekezaji wa Chuo cha Kilimo kwa Mkoa wa Lindi ni fursa kubwa kwenye uboreshaji na maendeleo ya kilimo hasa kupitia mazao ya korosho, ufuta, mbaazi, nazi na mazao ya chakula kwa ujumla.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.