• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

DKT. JAFO AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA ZAHANATI YA KIJIJI NGORONGOPA- LIWALE

Posted on: September 18th, 2024

Katika ziara maalum ya Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt Seleman Jafo (Mb) wilayani Liwale ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa zahanati mpya katika kijiji cha Ngorongopa hatua ambayo inatarajiwa kuboresha huduma za afya kwa wakazi wa kijiji hicho na maeneo jirani punde itakapokamilika ifikapo Novemba 30,2024.


Hatua hiyo imekuwa faraja kubwa kwa wananchi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakitembea umbali wa kilomita 10 kwenda kijiji jirani cha Nangirikiti hivyo ujenzi wa zahanati hiyo unakwenda kuleta afueni ya changamoto haswa za usafiri kwa wakazi hao hususan akina mama wajawazito, watoto wachanga na wazee.


Akisoma taarifa ya ujenzi wa zahanati hiyo iliyogharimu Tsh Milioni 50 kutoka serikali kuu, Bwana. Mbaraka Juguju, mtendaji wa kata ya Ngorongopa ameeleza kuwa ujenzi wa zahanati hiyo unakwenda kuwa tiba ya changamoto za huduma ya afya zilizokuwa zinawakabili wakazi wapatao 1219 huku ikisogeza karibu huduma za kujifungua na kliniki kwa wajawazito na watoto.


Dkt. Jafo amewahakikishia wananchi hao kuwa zahanati hiyo itaanza kutoa huduma mara tu ujenzi wake utakapokamilika.


"Niwahakikishie kuwa tayari serikali imeshatoa fedha kwa ajiri ya kununulia vifaa tiba na imeshaelekeza wahudumu wa afya watakaokuja kutoa huduma hapa, hivyo zahanati hii itaanza kufanya kazi mara tu ujenzi wake utakapokamilika Novemba 30 mwaka huu" ameeleza.


Bi. Hawa Abdallah, mama mwenye mtoto mchanga wa siku 9 alikuwepo kushuhudia tukio hilo na kueleza kuwa kabla ya uwepo wa zahanati hiyo wajawazito walikuwa wanachelewa kuanza mahudhurio ya kliniki pamoja na watoto wachanga kutokukamilisha ratiba ya chanjo mbalimbali kutokana na kukwepa gharama za usafiri kwenda Nangirikiti.


"Nina imani kubwa kuwa baada ya zahanati hii kufunguliwa, hatutakuwa na haja ya kutembea umbali mrefu. Wajawazito wataanza kuhudhuria kliniki kwa wakati na hatutolazimika kuwakatiza watoto wetu kupata chanjo zote zinazostahili kama inavyotakiwa. Tunaishukuru sana serikali ya Mama Samia na tunamuombea kwa Mungu ampe afya njema ili azidi kutuhudumia wananchi wake." ameeleza Bi. Hawa.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.