• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MKUU WA MKOA WA LINDI AMEWAPONGEZA WALIMU KWA MATOKEO MAZURI YA KIDATO CHA NNE

Posted on: February 17th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack ametoa pongezi hizo Jana Alhamisi katika kikao cha Idara ya elimu kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi. Kikao hicho kilichojumuisha wadau mbalimbali kulikuwa na lengo la kuwasilisha mpango mkakati wa Mkoa unaolenga kuongeza ufaulu wa wanafunzi kwa mwaka 2023. 


Pamoja na pongezi hizo , Mhe. Telack amesema kuwa Mkoa wa Lindi Kwa ujumla umefanya vzuri Sana kwenye matokeo ya kidato cha nne yaliyotoka mwaka huu, hivyo kuna haja sasa ya kuboresha mazingira ya walimu.

"Nitumie nafasi hii kuwapongeza walimu wanafunzi na wazazi wote kwa kazi nzuri na kubwa walioifanya.........ki ujumla matokeo ya kidato cha nne mkoa wetu umefanya vizuri sana". Amesema Mhe. Telack.


Mhe. Telack ametoa wito kwa wazazi na wadau kuunga mkono jitihada za walimu kwa kuboresha mazingira yao ya kufundishia pamoja na makazi. Amesisitiza kuwa wadau waunganishe nguvu kwa pamoja ili zijengwe nyumba za walimu na kuwapa nafasi ya kufanya kazi yao kwa utulivu. Pia amezitaka Halmashauri kutumia mapato ya ndani kujenga nyumba za walimu ili wautumie muda wao wa kazi vizuri.


Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Lindi Ndg. Ngusa Samike wakati akifungua kikao cha Maabara ya elimu kilichofanyika mwanzoni mwa wiki hii katika ukumbi wa Chuo cha Ualimu, Nachingwea amewataka walimu kuwafuatilia wanafunzi wanaoacha shule na kuingia mtaani na kujiingiza kwenye ajira za utotoni.


Ndg. Ngusa Ameongeza kuwa walimu wanatakiwa kuwasimamia watoto toka wanapoandikishwa darasa la awali na kuwafuatilia mpaka wanapohitimu shule kwa ngazi zote. 


Amewataka walimu wote kubuni mikakati madhubuti  itakayowavutia na kuwahamasisha wanafunzi kuendelea na masomo ili baadae Taifa liwe na wasomi wa kutosha.


Kwa upande wake, Afisa elimu Mkoa wa Lindi Ndg. Joseph Mabeyo amesema kuwa Mkoa unaendelea kushirikiana na wadau wote wa elimu ili kufikia malengo yaliyowekwa. Mkoa unaendelea kutekeleza na kubuni mikakati itakayotokomeza matokeo ya daraja sifuri kwa watahiniwa wa kidato cha nne. 


Ndg. Mabeyo ameongeza kuwa  idadi ya watahiniwa waliopata daraja sifuri kwa mwaka 2021 walikuwa 539 na mpaka kufikia mwaka 2022 idadi hiyo ilipungua na kufikia 334.


Jitihada za Walimu katika kuleta mapinduzi ya elimu kwa Mkoa wa Lindi zinaendelea kuzaa matunda   mazuri ambapo Kwa mujibu wa taarifa za Baraza la Taifa la Mitihani za mwaka 2019-2020, Mkoa wa Lindi umetajwa kuwa Mkoa pekee uliopandisha kiwango cha ufaulu kwa miaka mitatu mfululizo.













ReplyForward















Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.