• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

GIRLS EFFECT YAZINDUA MRADI WA WA CHANJO MKOANI LINDI

Posted on: July 21st, 2023

Shirika la kimataifa la Girls Effect linaloendesha shughuli zake kwa lengo kuu la kuwafikia vijana na taarifa sahihi kuhusu afya zao  siku ya Jumatano wiki hii, tarehe 19 Julai 2023 limezindua rasmi mradi wa uhamasishaji wa chanjo kwa watoto na wasichana Mkoani Lindi ujulikanao kama " Mwanzo Mwema".

Uzinduzi huo umefanyika Wilayani Nachingwea kwenye kikao Maalum kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Ualimu, TTC kikiwahusisha Viongozi wa Mkoa, Wilaya, Halmashauri, Viongozi wa dini pamoja na wadau wengine katika sekta ya elimu na afya.

Mradi huo unaofadhiliwa na GAVI the Vaccine Alliance utatekelezwa na Shirika la Girls Effect kwa muda wa miaka minne ambapo umeanza mwaka 2022 mpaka mwaka 2026 na utatoa huduma kwa watoto walio chini ya miaka miwili na wasichana wenye umri wa miaka 14  watanufaika katika Halmashauri za Liwale, Ruangwa, Kilwa na Nachingwea zilizopo Mkoani Lindi.

Kwa watoto walio chini ya miaka miwili, mradi utajikita kuhamasisha jamii kushiriki katika kuwapatia watoto hao chanjo zote muhimu. Pia mradi huo utahamasisha wasichana wa miaka 14 kupatiwa chanjo ya kuwakinga na saratani ya shingo ya kizazi, HPV pamoja na kuboresha tabia za ufuatiliaji wa mambo ya kiafya kwa jamii.

Utekelezaji wa mradi huu utafanyika kwa ushirikiano na Serikali kupitia Wizara ya Afya, Ofisi ya Rais-Tamisemi katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Katavi na Shinyanga.

Aidha,  Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe.Zainab Telack amelishukuru Shirika la Girls Effect kwa kuamua kuleta huduma zao Mkoani Lindi huku akiomba kuongeza wigo huduma hizo ikiwemo kwenye eneo la kuboresha masuala ya lishe.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Christopher Ngubiagai amesema kuwa katika utekelezaji wa mradi ni vyema Wakuu wa Wilaya husika wakashirikishwa vyema ili kuweza  kufikia malengo yaliyokusudiwa. 

























Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.