• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Hakikisheni watoto wanapata chanjo - DC Ndemanga

Posted on: September 24th, 2019

Hakikisheni watoto wanapata chanjo – DC Ndemanga

Mkuu wa wilaya ya Lindi, Mhe. Shaibu Ndemanga amewataka watendaji kuhakikisha kila mtoto chini ya miaka mitano anapata chanjo ya Surua-Rubela na Polio.

Mhe. Ndemanga ameyasema hayo katika kikao cha PHC cha ngazi ya wilaya na halmashauri ya manispaa ya Lindi kilichohusu kampeni ya kitaifa ya utoaji chanjo hiyo kwani kumekuwepo na tatizo la baadhi ya watu kutopeleka watoto kutopata chanjo kwasababu zao binafsi kunakosababisha magonjwa ya mlipuko kuendelea kujitokeza.

Serikali imekuwa ikifanya jitihada kubwa sana za kuhakikisha huduma za afya zinaboreshwa kwa wananchi ikiwa ni pamoja na utoaji wa chanjo kama hizi bure. Lengo ni kuzuia milipuko zaidi ya magonjwa hayo yanayoweza kujitokeza baada ya watu kushindwa kujitokeza na kushiriki kikamilifu katika kupata chanjo.

 “Niwaagize wataalam na watendaji wote mnaohusika na zoezi hili la utoaji chanjo kuhakikisha jamii inahamasishwa kujitokeza lakini pili asiwepo mtoto mwenye umri chini ya miaka mitano atakayekosa chanjo hii kwani suala hili sio la hiari na endapo atajitokeza mtu yeyote atakayebisha hatua kali zitachukuliwa dhidi yake kwa kuwa huyo atakuwa nanataka magonjwa yaendelee kujitokeza katika jamii yetu,” alisema Mhe. Ndemanga.

Aidha, Mhe. Ndemanga amewataka wataalam kuhakikisha katika zoezi la uhamasishaji jamii wahakikishe wanatoa elimu ya kutosha kwa jamii kuhusu umuhimu wa watoto kupata chanjo hiyo na madhara ya kutopata chanjo hiyo ili ieleweke vizuri. Lakini pia ameitaka jamii ya wanalindi kutambua kuwa zoezi hili litakuwa likisimamiwa pia na vyombo vya usalama lengo ni kuhakikisha linafanyika kikamilifu na kufikiwa malengo yaliyowekwa.

Naye mganga mkuu wa manispaa ya Lindi, Dkt. Dismass Masuluhu amesema chanjo hiyo itatolewa kwa watoto zaidi ya elfu 26 katika wilaya ya Lindi ambapo kutakuwa na siku tano za utoaji chanjo. Katika siku nne za mwanzo tutakuwa na maeneo maalum ya utoaji wa chanjo ambapo watu watatakiwa kufika katika vituo vyetu ili kupata chanjo na siku ya tano timu za Afya zitapita katika maeneo mbalimbali ya wananchi.

Dkt. Masuluhu amewaomba viongozi, wataalam mbalimbali na wadau waafya kushiriki katika kuhamasisha na kutoa elimu katika maeneo wanayotoka ili baadhi ya wananchi waache kuwa na imani potofu kuhusu chanjo hizo ambazo zinaatolewa na serikali kwa ajili ya kuwasaidia.

Mstahiki Meya wa manispaa ya Lindi, Mhe. Mohamedi Lidume amesema kuwa uhamasishaji mkubwa na utoaji wa elimu kwa jamii kutasaidia kuondoa uoga na imani potofu zilizojengeka ndani ya jamii.

Zoezi la utoaji chanjo ya Surua-Rubela na Polio kwa watoto chini ya miaka mitano katika manispaa ya Lindi linatarajiwa kuanza rasmi tarehe 15/10/2019 na kufika tamati tareha 19/10/2019.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.