• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE (LAAC) HAIJARIDHISHWA NA UENDESHAJI WA MFUKO WA MIKOPO YA 10%

Posted on: March 25th, 2023

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Serikali imeoneshwa kutoridhishwa na Usimamizi na uendeshaji wa Mfuko wa Mikopo ya Akina mama, Vijana na Watu Wenye Ulemavu inayotolewa na Halmashauri.


Hayo yamesemwa jana ijumaa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Halima Mdee(Mbunge) kupitia  hotuba yake ya ukaguzi  katika kuhitimisha ziara ya ukaguzi wa Miradi mbalimbali ya  maendeleo iliyofanyika  katika Wilaya za Nachingwea na Lindi.


Akisoma hotuba hiyo mbele ya wajumbe waliohudhuria kikao cha majumuisho kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Mdee ameeleza kuwa Halmashauri zina udhaifu katika Usimamizi na Uendeshaji wa Mfuko wa Mikopo ya Akina Mama, Vijana na Watu wenye Ulemavu.


Mhe. Mdee ameainisha kuwa udhaifu mkubwa upo kwenye urejeshaji wa Mikopo inayotolewa kwa makundi hayo matatu ambapo Kwa mwaka 2016/17 hadi 2020/21 Halmashauri ya Wilaya ya Mtama ilitoa kiasi cha TSH. 271.1 milioni na kufanikisha kurejesha Tsh. 121.7 milioni. Manispaa ya Lindi Kwa mwaka 2015/16 hadi 2020/21 ilitoa Mikopo kiasi cha TSH. 228.7 milioni na kufanikisha kurejesha kiasi cha TSH. 99.5 milioni. Kwa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea kwenye eneo la Mikopo, Mwenyekiti wa Kamati amesema kuwa Halmashauri ilikikopesha kikundi cha Akina mama kiitwacho Mshikamano kiasi cha TSH. 18 mil lakini kikundi hicho kimerejesha Tsh. 550,000 Tu.


Mhe. Mdee ameendelea kusema kuwa Mikopo hii ya Akina mama, Vijana na Watu wenye Ulemavu inatolewa bila kuzingatia uwiano wa asilimia 40:40:20.


Mhe. Mdee ameitaka Ofisi ya Rais TAMISEMI kufanya tathmini upya juu ya utaratibu wa kisheria na muundo wa kitaasisi utakaowezesha Usimamizi na uendeshaji bora wa Mfuko huu ili uweze kuleta tija kwa makundi yaliyokusudiwa na kuweza kujikwamua na wimbi la umaskini.


Maeneo mengine yalioanishwa kuwa na changamoto ni pamoja na ukusanyaji wa mapato ya ndani, kutokuzingatia miongozo ya Serikali katika matumizi ya mapato ya ndani, uchangiaji mdogo wa mapato ya ndani kwenye Miradi, uchache wa watumishi, pamoja na Usimamizi wa Miradi ya Serikali.


Kwa upande wake, Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Deogratius Ndejembi amesema kuwa kutokana na changamoto za urejeshwaji wa Mikopo TAMISEMI imeunda mfumo ambao utavisajiri vikundi na kutoa Mikopo Kwa mfumo huo. Mchakato unaendelea na TAMISEMI imeunda timu ambayo anafanya kazi kuona mfumo mzuri ambao utatumika.


Mhe. Deogratius Ndejembi ameongeza kuwa changamoto ya uchache wa watumishi, Serikali inalifanyia kazi na tayari Serikali imetoa kibali cha ajira za Wahandisi 260.


Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Shaibu Ndemanga ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Lindi ameipongeza Kamati hiyo kwa kazi nzuri waliofanya Mkoani Lindi na kuahidi kushughulikia changamoto zote zilizoelezwa na Kamati.


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa imehitimisha ziara ya ukaguzi wa Miradi  ya Serikali Mkoani Lindi ambapo  imefanya kazi hii kwa muda wa siku tatu tangu tarehe 21 Machi 2023.

























Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.