• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Kaswa afungua warsha ya utengenezaji Mpango wa motisha kwa ajili ya kuwavutia na kuwabakisha watumishi katika vituo vyao vya kazi.

Posted on: November 3rd, 2017

Kaswa afungua mafunzo ya kutengeneza Mpango wa motisha kwa ajili ya kuwavutia na kuwabakiza watumishi katika vituo vyao vya kazi.

Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Ndg. Ramadhani Kaswa amefungua warsha yenye lengo la kutengeneza mpango wa motisha kwa ajili ya kuwavutia na kuwabakiza watumishi katika vituo vyao vya kazi yanayofanyika katika Hotel ya M.M iliyopo Manispaa ya Lindi.

Warsha hii inayofanyika kwa siku sita imeandaliwa na serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo kupitia Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) ambapo washiriki ni Wakuu wa Idara za Rasilimali Watu, Elimu (Msingi na Sekondari), Mifugo, Mipango, Katibu wa Afya, Maafisa Utumishi, Watendaji wa Kata (hawa ni kwa Halmashauri za Kilwa na Ruangwa ambazo zipo chini ya mradi). Halmashauri nyingine za Lindi, Manispaa ya Lindi, Liwale na Nachingwea wameshiriki Maafisa Utumishi.

Kaswa alisema kuwa lengo la warsha hii ni kuandaa mikakati ya kutoa motisha na vivutio kwa watumishi katika Halmashauri jambo litakalopelekea watumishi kuwa na motisha na tija katika kutekeleza mjukumu yao. Pamoja na hilo lengo kuu ni kuwafanya watumishi kushawishika kuendelea kubaki kwenye vituo vyao vya kutolea huduma hai itakayochangia katika upatikanaji wa huduma bora na endelevu kwa wananchi.

“Ni matarajio yangu kuwa jambo hili likifanikiwa Mamlaka za Serikali za Mitaa zitakuwa na uwezo sio tu wa kuwabakisha watumishi wanaopangiwa bali pia kuinua kiwango cha ubora wa huduma zinazotolewa kwa wananchi katika sekta za elimu, afya, kilimo, mifugo, huduma za ardhi na maeneo mengine ya huduma”, alisema Kaswa.

Serikali ilishaona umuhimu wa jambo hili ndio maana ilipoandaa na kutunga Sera ya Malipo ya Mishahara na Motisha kwa Watumishi wa Umma ya mwaka 2011 suala hili la motisha lilibainishwa ikiwa ni pamoja na tafiti zilizofanyika ili kubaini maeneo yenye changamoto zaidi. Lakini kutokana na changamoto mbalimbali zilizojitokeza zikiwemo uchache wa fedha na mwamko mdogo wa baadhi ya viongozi kwenye maeneo husika katika kutimiza majukumu yao ambazo zilisababisha mafanikio tarajiwa kutofikiwa.

Kaswa alisema kuwa serikali inatambua umuhimu wa kuendeleza uboreshaji mazingira ya kazi kwa watumishi na ndio sababu ya uwepo wa warshaa hii ili kusifufua juhudi zilizokuwepo. Hii ni kutokana na watumishi baadhi wanaopangiwa kazi katika vituo mbalimbali kuacha kazi au wengine wanasingizia kuwa na matatizo ili wahame kutokana na changamoto wanazozikuta kwenye vituo vya kazi.

Pia ameishukuru Serikali ya Marekani kupitia shirika lake la USAID kwa kuunga mkono jitihada hizi kama ambavyo wamekuwa wakiunga mkono katika maeneo mengine mengi ya maendeleo. Aidha, amewasihi washiriki kuhakikisha wanaandaa mikakati ya motisha kwa kuzingatia sababu zilizopelekea mikakati ya zamani kushindwa kufikia malengo yake. Vilevile amewasisitiza kuhakikisha katika mipango wanayoipanga wahakikishe kwanza ni ile inayotekelezeka ndani ya Halmshauri zao bila kusahau kubainisha wadau husika na namna watakavyoshiriki.

Serikali inaendelea kushughulikia changamoto mbalimbali wanazokutana watumishi walio katika mazingira magumu kwa kadri uwezo unaporuhusu.

Aidha, tukumbuke kuwa suala la kutoa motisha kwa watumishi litakuwa na maana kama litakuwa ni endelevu, hivyo ni vema mipango mtakayotoka nayo hapa na kwengineko ijengwe ndani ya mifumo ya utendaji wa Halmashauri, ili iwe rasmi, endelevu na kuingizwa katika mifumo ya ufuatiliaji na uwajibikaji.

Mmoja wa waratibu wa mafunzo haya Bi. Restituta Masao ambaye alitoa maelezo mafupi kuhusu warsha hii alisema kuwa mpango mkakati huu utaandaliwa kwa kuzingatia hali ya kiutumishi na hali ya mazingira husika ili kuweza kuibua changamoto na kuzitafutia ufumbuzi. Pia alieleza kuwa katika mpango utakaoandaliwa utaainisha majukumu ya kila mdau kwani hii itasaidia katika usimamizi na ufuatiliaji wa utekelezaji wa mpango.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.