• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MADAKTARI BINGWA WA RAIS SAMIA WAOKOA MAISHA YA MJAMZITO RUANGWA

Posted on: September 18th, 2024

Kambi ya Madaktari Bingwa na Ubingwa Bobezi wa Rais Samia inayoendelea katika mkoa wa Lindi imeokoa maisha ya mama mjamzito ambaye mimba yake ilitungwa nje ya mji wa mimba kwa kumfanyia upasuaji katika Hospitali ya Wilaya ya Ruangwa.


Upasuaji huo umefanyika Septemba 17, 2024 katika Hospitali ya Wilaya Ruangwa ukiongozwa na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya wanawake uzazi na Watoto Dkt. Lilian Mnabwiru kwa mgonjwa aliewasili hospitalini hapo akiwa katika hali ya hatari na kuhitaji kufanyiwa upasuaji wa Dharura.


“Kuna mama ambae alikuwa anatokwa damu ndani kwa ndani kwasababu mimba yake ilitungwa nje ya mji wa mimba tulimkuta katika hali mbaya kwani damu nyingi ilikuwa imepotea pressure imeshuka na hivyo alikuwa katika hali mbaya sana.” Amesema Dkt. Mnabwiru


Dkt. Mnabwiru ameendelea kusema kuwa mimba kutungwa nje ya mji wa mimba ni hatari kwa mama na mtoto kwani mtoto atakosa mahitaji muhimu katika ukuaji wake lakini walifanikiwa kuondoa kiumbe kilichojipandikia na kuzuia damu iliyokuwa inavuja ndani ya tumbo.


“Tulitoa damu takribani lita mbili na nusu zilizovujia tumboni na kumuongezea damu nyingine kurudisha ile iliyopotea. Mgonjwa ameshaamka na anaendelea vizuri kwa sasa.” Amesema Dkt. Mnabwiru


Kwa upande wake, Bi Maua Ally ambaye ni mdogo wa mgonjwa huyo amewashukuru Madaktari bingwa wa Rais Samia kwa kuokoa maisha ya dada yake kwani hali yake ilikuwa mbaya sana lakini kwa jitihada zao zimerejesha matumaini kwa Mgonjwa.


“Mgonjwa alipoteza fahamu kabisa lakini tulivyofika hapa tumekutana na maktari bingwa wamemuhudumia na sasa haliyake imeimarika.” Amesema Bi. Maua


Kambi hii ya Matibabu ya Madaktari Bingwa wa Rais Samia inaendelea Mkoani lindi katika Hospitali zote za Wilaya hivyo wananchi wanahimizwa kwenda Hospitalini kwani huduma za Kibingwa na Ubingwa Bobezi zimesogezwa karibu kwa lengo la kupunguza gharama kubwa  za kufuata Huduma hizo kwenye Hospitali za Kanda na Rufaa.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.