• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mgogoro wa mpaka kati ya Kijiji cha Nanjilinji A na Kijiji cha Mirui kutatuliwa

Posted on: July 9th, 2018

Mgogoro wa mpaka kati ya Kijiji cha Nanjilinji A na Kijiji cha Mirui kutatuliwa

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi amesema amekuja Lindi na majibu ya utatuzi wa mgogoro wa mpaka wa kijiji cha Nanjilinji A na Kijiji cha Mirui.

Mhe. Lukuvi ameyasema hayo leo kabla ya kuanza kikao kilichowajumuisha wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Wilaya za Kilwa na Liwale. Pia katika kikoa hicho walishiriki Wakuu wa Wilaya za Lindi na Ruangwa pamoja na wataalam toka wizara ya ardhi, mkoa na halmashauri za wilaya husika.

“Leo tumekuja na majibu ya mgogoro wa mpaka uliopo kati ya Kijiji cha Nanjilinji A kilichopo Wilaya ya Kilwa na Kijiji cha Mirui kilichopo Wilaya ya Liwale baada ya timu ya Wataalam kupitia nyaraka mbalimbali zilizotumika katika uanzishwaji wa Wilaya na Vijiji hivyo”, alisema Mhe. Lukuvi.

“Licha ya kutatua mgogoro huo, wizara kwa kushirikiana na mkoa na wilaya watapima na kuweka alama za kudumu (mawe) za mipaka katika vijiji hivyo ikiwa ni pamoja na kuwatengenezea mpango wa matumizi bora ya ardhi”, aliongeza Mhe. Lukuvi.

Aidha, Mhe. Lukuvi amesema kuwa wizara imejipanga kuhakikisha inaboresha ofisi zake za kanda ambapo kwa kanda ya kusini maafisa wote muhimu wameshapelekwa na vifaa vya kazi vitawasili mwezi Agost, 2018. Hivyo shughuli nyingi zinazohusu masuala ya ardhi zitakuwa zinamalizika katika ofisi za kanda na sio wizarani kama ilivyokuwa awali.

Kutokana na maboresho hayo ya ofisi za kanda, Mhe. Lukuvi amesema kwamba wizara inatarajia kwamba halmashauri katika kanda husika zitahakikisha vijiji vyote vinapimwa, mpango wa matumizi bora wa vijiji unaandaliwa na wananchi wenye ardhi wanamilikishwa kwa kupatiwa hati.

Mhe. Lukuvi amepongeza jitihada zinazofanywa na mkoa chini ya Mkuu wa Mkoa, Mhe. Godfrey Zambi za kuhakikisha migogoro ya ardhi iliyopo inatatuliwa, na kwamba ni imani yake kuwa Mkoa unaweza kumaliza migogoro iliyopo kabla ya muda uliowekwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Awali  Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi akimkaribisha  waziri lukuvi , alisema mkoa unaendelea kufanya jitihada mbalimbali katika kumaliza migogoro ya ardhi iliyopo. Ambapo pia alitaja baadhi ya migogoro hiyo kuwa ni wananchi kuvamia shamba la Mauhumbika (Mahumbika Plantation), Shamba la Mkwaya katika Wilaya ya Lindi, mgogoro wa mpaka kati ya wananchi na Kikosi namba 843 jeshi la wananchi JWT na Kikosi 41 JKT vya jeshi la kujenga taifa  ambavyo vipo katika Wilaya ya Nachingwea.

Vilevile aliuelezea mgogoro wa mpaka uliopo wa kijiji cha Nanjilinji A – Kilwa na kijiji cha Mirui – Liwale. Migogoro mingine iliyopo sio mikubwa sana ambapo mkoa kwa kushirikiana na wilaya imekuwa ikiendelea kuchukua hatua mbalimbali katika kuitatua.

Mhe. Zambi amempongeza waziri kwa kazi nzuri anayoifanya katika wizara hasa katika kutatua migogoro ya ardhi iliyopo pamoja na kuongeza wataalam katika ofisi za kanda ili kusogeza upatikanaji wa huduma za masuala ya ardhi jirani na wananchi.

Mhe. Lukuvi licha ya kufanya mkutano na wajumbe wa kamati za ulinzi na usalama, pia mchana atasikiliza malalamiko ya masuala ya ardhi toka kwa wananchi wa manispaa ya Lindi na maeneo ya jirani na kuyatolea ufumbuzi. Aidha, kesho tarehe 10 Julai, 2018 atakwenda katika Kijiji cha Mirui na Kijiji cha Nanjilinji A ambapo katika maeneo yote hayo atazungumza na wananchi kuwaelezea hali halisi ya mipaka ilivyo na mpango uliopo katika kumaliza mgogoro uliopo.

BAADHI YA PICHA ZA VIKAO ALIVYOFANYA MHE. LUKUVI.



Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.