• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mhe. Lukuvi azitaka Halmashauri kuongeza ukusanyaji wa Maduhuli

Posted on: May 4th, 2017

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe William Lukuvi amezitaka Halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya kuhakikisha zinaongeza ukusanyaji wa maduhuli kwani kwa sasa yapo chini sana.

Mhe. Lukuvi ambaye amefanya ziara ya siku moja Mkoani Lindi katika Wilaya ya Lindi alisema kuwa bado hali ya makusanyo ya maduhuli na kodi za ardhi yapo chini ukilinganisha na malengo Mkoa uliojiwekea. Ambapo kwa mwaka 2016/2017 Mkoa ulikuwa na lengo la kukusanya 3,270,000,000.

Lakini mpaka tarehe 27 Aprili 2017 Halmashauri za Wilaya na Manispaa zilikuwa zimekusanya shilingi 2,245,090,359 ikiwa ni asilimia 68.66 ya lengo la makusanyo. Hivyo Mhe. Lukuvi amezitaka Halmashauri zote kuhakikisha ifikapo tarehe 30 Juni 2017 zimekamilisha kukusanya kiasi kilichobakia.

Pia ameziagiza Halmashauri kuongeza kasi ya upimaji wa viwanja na mashamba ikienda sambamba na umilikishaji wake kwani kwa kufanya hivyo ndio kutato fursa kwa wananchi wamiliki wa ardhi kuweza kukopesheka kwenye mabenki. Vilevile kuuweka mji katika mpangilio unaoeleweka.

“Kwa kutopima viwanja mnafanya mji kujengwa kiholela hivyo ukatazaji watu kujenga kiholela uende sambamba na kasi ya upimaji maeneo na umilikishaji”, alisema Mhe. Lukuvi. Vilevile aliwaagiza Watendaji wa Kata na Mitaa katika miji kuhakikisha wanatoa taarifa pale wanapoona ujenzi wa kiholela unapotaka au kuanza katika maeneo yao ili hatua zichukuliwe kwa wakati.

Aidha, amempongeza Mhe. Zambi kwa kazi kubwa anayoifanya ya kutatua migogoro ya ardhi katika mkoa na kumuahidi kuwa yeye pamoja na Wizara wataendelea kutoa ushirikiano pale utakapohitajika. Vilevile aliuagiza Mkoa kuyapitia upya mashamba yote yasiyoendelezwa na kujua kama yanalipiwa kodi. Pia kujua kama kuna hatua zozote ambazo zimechukuliwa na kama bado basi wahusika wapewe ilani na taarifa hiyo apatiwe.

Pia Mhe. Lukuvi amesema tayari wameshatangaza katika gazeti la serikali uanzishaji wa mabaraza ya ardhi katika Wilaya ya Ruangwa na Nachingwea. Lakini amekubali kwenda kulifanyia kazi ombi la Mkuu wa Mkoa la kuanzisha mabaraza ya ardhi katika Wilaya ya Liwale na Kilwa kutokana na umbali uliopo kufika Lindi ambako kwa sasa ndio lipo baraza la ardhi.

Katika taarifa ya Mkoa iliyosomwa kwake na Katibu Tawala Mkoa, Ndg. Ramadhani Kaswa ilibainisha maendeleo ya sekta ya ardhi. Ambapo ilibainisha masuala ya hali ya watumishi, maeneo ya uwekezaji mkubwa, upimaji wa ardhi na viwanja, uandaaji wa hati miliki za viwanja na hatimiliki za kimila, ukusanyaji wa maduhuli na kodi za ardhi na utengaji wa maeneo ya viwanda na maeneo ya wajasiriamali.

Pamoja na taarifa hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zambi alimueleza Waziri kuwa Mkoa bado unaendelea kushughulikia migogoro ya ardhi ambapo aliitaja baadhi ya migogoro kama; mgogoro wa mpaka kati ya Lindi na Mtwara, mgogoro wa mpaka kati ya Kilwa na Rufiji, na migogoro ya mpaka kati ya wananchi na JWTZ katika Wilaya za Kilwa, Lindi na Nachingwea. Migogoro yote hii inaendelea kushughulikiwa katika ngazi ya mkoa.

Mhe. Lukuvi alitembelea na kukagua mfumo wa makusanyo ya kodi za ardhi katika masijala za ardhi zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Lindi na Manispaa ya Lindi. Ambapo pia aliendelea kusisitiza Halmashauri ziongeze kasi ya upimaji, utoji hati na ukusanyaji wa maduhuli na kodi za ardhi.

Vilevile alitembelea ofisi za Shirika la Nyumba ambapo baada ya kupata taarifa, Mhe. Lukuvi aliwashauri katika majengo yao yaliyochoka waanze kuangalia uwezekano wa kuwapata wadau ambao watashirikiana nao katika kuwekeza kwenye maeneo hayo. Hapa pia alimwagiza mkurugenzi wa manispaa kuhakikisha wanawapa ilani wale wote wenye majengo chakavu katika miji na kuanza kutoa vibali vya ujenzi wa aina ya majengo kulingana na mpango wa matumizi ya ardhi wa eneo husika.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.