• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mhe. Lukuvi: Wananchi msibadilishe matumizi ya msitu wa Mbumbilaa

Posted on: July 11th, 2018

Mhe. Lukuvi: Wananchi msibadilishe matumizi ya msitu wa Mbumbilaa

Wananchi wa kijiji cha Nanjilinji A na kijiji cha Mirui wameagizwa kutobadilisha matumizi ya ardhi ya msitu wa Mbumbilaa ambao awali ulikuwa unamilikiwa na kijiji kimoja.

Maagizo haya yametolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi wakati alipotembelea vijiji hivyo kwa ajili ya kutao ufafanuzi kuhusu mgogoro wa mpaka wa ardhi uliopo kati ya kijiji cha Nanjilinji A kilichopo wilaya ya Kilwa na kijiji cha Mirui kilichopo wilaya ya Liwale ambapo aliwaeleza wananchi hatua ambazo zitachukuliwa ili kumaliza mgogoro huo.

Msitu huu wenye ukubwa wa hekta 64,000 awali ulikuwa unamilikiwa na kijiji cha Nanjilinji A lakini baada ya wataalam kupitia upya ramani zilizopo, wakabaini kwamba asilimia 30 ya msitu huu ipo katika kijiji cha Mirui. Mhe. Lukuvi aliwaeleza kuwa mpaka utakaowekwa utaonyesha eneo hilo na kwamba kuanzia sasa kijiji cha Mirui kitaanza kunufaika na msitu.

“Kwa kuwa wataalam wamebaini kuwa asilimia 30 ya msitu wa Mbumbilaa upo ndani ya kijiji cha Mirui, kuanzia leo tarehe 10/07/2018 kijiji cha Mirui kitaanza kunufaika na mapato yatokanayo na msitu wa huu kulingana na asilimia ya msitu uliopo katika kijiji cha mirui”, alisema Mhe. Lukuvi.

“Aidha, ni marufuku kwa kijiji cha Mirui na Nanjilinji A kubadilisha matumizi ya msitu wa Mbumbilaa, eneo la msitu ni lazima liendelee kulindwa na pande zote za vijiji kwa kuzingatia mipaka mtakayoonyeshwa na wataalam kwa mujibu wa ramani”, alisisitiza Mhe. Lukuvi.

Katika kutatua mgogoro huu wa mpaka, ilibainika kuwa mpaka wa vijiji hivyo vya mpakani kwa mujibu wa tangazo la serikali la mwaka 2007 ulikuwa umekosewa kwa kutozingatia mipaka ya kiwilaya na hivyo unatakiwa kufanyiwa marekebisho kwa kufuata tangazo la serikali la mwaka 1980 iliyotangaza mpaka kati ya wilaya ya Kilwa na Liwale. Hivyo ramani ya kijiji cha Mirui inatakiwa kurekebishwa kwa kutengenezwa nyingine pamoja na hati wakati ramani ya kijiji cha Nanjilinji A inatakiwa kutengenezwa mpya kwani kijiji hakina ramani wala hati.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi amewasihi wananchi katika vijiji hivi kuhakikisha wanawapa ushirikiano wataalam wa ardhi ambao watakwenda kuweka alama za mipaka.  Aidha, amewataka Wakuu wa Wilaya za Kilwa na Liwale pamoja na wakurugenzi kuhakikisha wanasimamia kuhakikisha alama za mipaka, upimaji na upatikanaji wa hati linaanza kutekelezwa tarehe 20 Julai 2018.

Pia Mhe. Zambi amemuhakikishia Waziri kuwa mkoa utaendelea kushughulikia malalamiko na kutatua migogoro ya ardhi iliyopo na kuhakikisha utaratibu unawekwa ili kuzuia migogoro mipya isijitokeze.

Wananchi katika vijiji vyote viwili walikubaliana na maelezo ya waziri kuhusu utatuzi wa mgogoro wa mpaka. Aidha, wananchi wa pande zote mbili wamempongeza juhudi kubwa zilizofanywa na wizara, mkoa na wilaya katika kutatua mgogoro huu uliodumu kwa muda mrefu.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.