• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mhe. Mwakyembe: Hongereni wanalindi

Posted on: October 26th, 2018

Mhe. Mwakyembe: Hongereni wanalindi

Wananchi wa mkoa wa Lindi wamepongezwa kwa kutunza na kuhifandhi mila, desturi na utamaduni wao.

Pongezi hizi zimetolewa na Mhe. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo alipokuwa akifungua tamasha la utamaduni wa watu wa Lindi kwa niaba ya Mhe. Samia Suluh Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani lililofanyika katika kijiji cha makumbusho mkoani Dar es Salaam.

Mhe. Mwakyembe alisema kuwa wanalindi kupitia tamasha hili la utamaduni wamefanikiwa kuonyesha mambo mbalimbali ya kiutamaduni. Pamoja na pongezi hizo, amewasihi wanalindi kuhakikisha wanaendelea kuzitunza tamaduni hizi kwa kuvirithisha vizazi vya sasa na vijavyo ili zisipotee.

“Wanalindi sasa inatakiwa mjipange kuhakikisha mnazitumia shughuli hizi za kiutamaduni kwa maendeleo ya mkoa na taifa kwa ujumla kwani hii inaweza kuwa ni fursa hata kwa watalii kuja kuona shughuli na kazi za kitamaduni zinazofanyika”, alisema Mhe. Mwakyembe.

“Serikali itaendelea kutunza, kulinda na kuhifadhi tamaduni za watanzania lakini hata wananchi wanao wajibu wa kuhakikisha tamaduni zetu zinatunzwa na kuendelezwa kwa manufaa ya vizazi vijavyo” alieongeza Mhe. Mwakyembe.

Aidha, ameupongeza uongozi wa Mkoa, ukiongozwa na Mhe. Godfrey Zambi, Mkuu wa Mkoa kwa dhamira njema ya kufanya tamasha la utamaduni na uendelezaji michezo. Pia ameipongeza wilaya ya Ruangwa kwa kujenga uwanja wa mpira wa miguu “Majaliwa Stadium” uliopo wilayani humo. Ujenzi wa uwanja huu ni fundisho kubwa hata kwa timu zetu ambazo zimekuwa zikicheza ligi kuu kwa miaka mingi lakini mpaka sasa hazijajenga kiwanja.

Kabla ya kumkaribisha waziri, Mhe. Zambi alisema kuwa tamasha lina wawakilishi kutoka katika kila halmashauri ambao wataonyesha shughuli mbalimbali za kitamaduni (zikiwemo ngoma, zana za asili, vyakula nk.) zilivyo katika maeneo yao.

Pia alitoa taarifa fupi ya hali ya maendeleo katika mkoa iliyoainisha vivutio vya kihistoria katika sekta ya utalii ambavyo unaweza kuvipata ukitembelea tovuti ya mkoa http://www.lindi.go.tz/economic-activity/utalii

Mhe. Zambi amemuhakikishia waziri kuwa mkoa umejipanga kuhakikisha kupitia tamasha hili watanzania wanapata fursa ya kuuelewa vizuri mkoa wa Lindi kwa kuanzia kwenye tamaduni zake. Aidha, alitumia fursa hii kuwakaribisha wawekezaji kuwekeza katika mkoa wa Lindi kwani mkoa huo unazo fursa nyingi za kiuchumi. Pia aliwahakikishia wawekezeji kuwa viongozi na wananchi wapo tayari kutoa ushirikiano kwa yeyote yule atakayekuwa tayari kwenda kuwekeza.

Naye mwenyeji wa tamasha hili, Ndg. Mpanda alisema kuwa matamasha kama haya yanatoa fursa kwa watanzania kuweza kujifunza tamaduni za maeneo mengine na hivyo kuzidi kuimarisha mshikamano wetu. Pia amewaomba watanzania hasa wanaoishi Dar es Salaam kufika kwa wingi kujione mambo mbalimbali ya tamaduni za watu wa Lindi.

Mkurugenzi mkuu wa makumbusho ya taifa, Prof. Audax Mabulla amesema kuwa tamasha hili ni la 27 kufanyika katika kijiji cha makumbusho. Lakini kwa kuwa sasa kijiji cha makumbusho kinajengwa kwa kufuata ramani ya Tanzania, mkoa wa Lindi ndio umekuwa wa kwanza kujenga nyumba kwa kuzingatia hilo. Pia amewapongeza wanalindi kwa kufika kwa wingi na kuonyesha shughuli mbalimbali za kitamaduni.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.