• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MHE. NDERIANANGA AZITAKA KAMATI ZA MAAFA MKOANI LINDI KUJIPANGA KUKABILIANA NA MAJANGA.

Posted on: November 21st, 2023

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Hamis Nderiananga amezitaka kamati zinazoshughulikia maafa Mkoani Lindi kuendelea kupanga mikakati madhubuti katika kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na maafa sambamba na kukumbusha wajibu wa taasisi za kisera na taasisi katika kuchukua hatua za kuokoa maisha na mali za wanajamii.

Naibu Waziri ameyasema hayo alipokuwa akifungua kikao kazi cha kujenga uwezo kwa Kamati za Usimamizi wa Maafa mkoani Lindi kilichoratibiwa na Idara ya Menejimenti ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu ambapo kimelenga kuzifikia kamati za maafa kwa ngazi za mikoa na kuzijengea uwezo wa kukabiliana na maafa  pindi yanapotokea  ambapo Mhe.  Ummy amezikumbusha kamati hizo umuhimu wa kujiandaa na kukabiliana na maafa kwa kuzingatia madhara yatokanayo na maafa hayo.

"Kikao chetu cha leo kimezingatia wajibu mlionao kwa kuzingatia mujibu wa sheria ya Usimamizi wa Maafa namba 6 ya mwaka 2022 na kanuni zake, ambayo imeanzisha Kamati za Usimamizi wa Maafa za Mikoa, Wilaya,Kata na Vijiji huku Jukumu la msingi la kamati hizo nikuchukua hatua kwa lengo la kuzuia na kupunguza madhara ya majanga ya aina zote na kujiandaa kwa lengo la kukabiliana na kurejesha hali ya awali kwa ubora zaidi endapo maafa yatatokea" Alieleza.

Aidha, Naibu Waziri amekumbushia wajibu wa kila mmoja katika eneo lake la kazi kuendelea kuchukua hatua stahiki endapo maafa yatatokea huku akielezea kuwa mfumo wa serikali unatambua na kuzingatia wajibu wa sekta binafsi na taasisi zenye jukumu kisera na kisheria katika kuchukua hatua stahiki ili kuokoa maisha na mali za jamii.

"Uzoefu unaonyesha kuwa kuchukua hatua za mapema ili kuzuia au kupunguza madhara zimekuwa na gharama nafuu kuliko kusubiri na kuchukua hatua pale maafa yanapotokea ambapo serikali imekuwa ikilazimika kutumia pesa nyingi na hapa nipongeze juhudi na hatua hizi za mapema zinazofanywa na serikali chini ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuimarisha uchumi na huduma za kijamii katika ujenzi wa Taifa letu zinakuwa stahimilivu dhidi ya maafa" Mhe. Ummy Nderiananga.

Aidha, Mhe.Shaibu Ndemanga, Mkuu wa Wilaya ya Lindi akitoa salamu za Mkoa wa Lindi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi ameeleza kuwa Mkoa umeendelea kujipanga na kuchukua hatua zote za tahadhari  katika kukabiliana na maafa mbalimbali ikiwemo tahadhari za mvua za Elnino zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini kama ilivoelekezwa na Mamlaka ya Utabiri wa Hali ya Hewa, na kuhaidi kuendelea kuzingatia umuhimu wa kuchukua tahadhari za mapema.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.