• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MHE. TELACK AKABIDHI MAGARI 18 KWA IDARA YA AFYA

Posted on: December 5th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack amekabidhi rasmi magari 18 yaliyotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuboresha huduma za afya katika mikoa ya Tanzania ikiwemo Mkoa wa Lindi.

Akikabidhi magari hayo, Mhe.Telack amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokana na anavyowajali wananchi wa Mkoa wa Lindi kwa kuwapatia jumla ya magari 18 ya kisasa ambapo magari 10 yatatumika kwa shughuli za ufuatiliaji na magari 8 yatatumika kubebea wagongwa (ambulance) .

Mhe. Telack amesisitiza kuzingatia matumizi mazuri ya magari hayo ambayo yametengenezwa maalum kwa kusafirisha na kutoa huduma kwa mgonjwa kwa kiwango cha hali ya juu.

Awali, akitoa taarifa ya Mkoa, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Dkt. Kheri Kagya amepongeza juhudi na dhamira nzuri ya serikali ya awamu ya sita katika kuhakikisha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi kwa kuboresha upatikanaji wa vifaa tiba pamoja na ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya kutolea huduma hizo.

Dkt. Kagya ameendelea kueleza kuwa vifaa tiba hivyo vinaenda kuhakikisha upatikanaji wa huduma za vipimo na matibabu ambayo awali havikua vinapatikana katika hospitali za wilaya na rufaa ndani ya mkoa ikiwemo Huduma za vipimo vya mionzi ya CT-Scan, Ultrasound, X-ray pamoja na mashine 10 za usafishaji wa damu yaani Dialysis Machine ambazo hutumika hususan kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo.

Vilevile, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi ameishukuru na kupongeza juhudi endelevu za kuboresha huduma za afya ikiwemo na uletwaji wa magari 18 katika mkoa wa Lindi ambayo yanahusisha na magari ya kubebea wagonjwa (ambulance) ya kisasa yenye uwezo na vifaa vinavyowezesha utoaji huduma za dharula kwa wagonjwa.

Makabidhiano hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya na Mkoa wakiwemo Wabunge, Wakuu wa wilaya, Wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi ambapo wote wametilia mkazo kuhusu usimamizi na matumizi sahihi ya magari hayo katika kuboresha huduma za afya kwa wanajamii.


Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.