• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MHE: TELACK AWATAKA WAKULIMA WA MWANI KUJIWEKEA AKIBA YA PEMBEJEO

Posted on: February 1st, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack amewataka wakulima wa mwani Mkoa wa Lindi kubadili fikra tegemezi ili waweze kujisimamia kwenye mahitaji ya pembejeo.

Mhe. Telack ameyasema hayo Leo katika kongamano la Uvuvi lililofanyika Wilayani Kilwa baada ya kuibuka hoja ya mgongano Kati ya wanunuzi na wakulima wa zao hilo. Changamoto hiyo inasababishwa na wakulima wa zao hilo kukiuka mkataba unaowataka kumuuzia mazao ya mwani mnunuzi aliyewapatia pembejeo kwa ajili ya uzalishaji wa zao hilo. Hivyo baadhi ya wakulima baada ya kuvuna mwani huwauzia wanunuzi wengine tofauti na mnunuzi aliyeingia mkataba na wakulima hao kwa kuwapatia pembejeo.

Kutokana na changamoto hiyo, Mhe. Telack amewataka wakulima kubadilika na waanze kujiwekea fedha benki kidogo kidogo zitakazo wawezesha kununua pembejeo zao wenyewe. Ameongeza kuwa kwa kufanya hivyo itasaidia kupanda Kwa bei ya zao hilo ambapo Kwa Wilaya ya Kilwa ni Tsh. 1,000/= Kwa kilo moja.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa mtandao usio wa kiserikali, LANGO Ndg. Michael Mwanga amesema kuwa taasisi hiyo imewasaidia wakulima wa mwani wa Mkoa wa Lindi kwa kuwapatia zana za Kilimo hicho ikiwemo kamba, taitai pamoja na viatu vya cha-cha-cha zenye thamani ya Tsh.32,400,000. Ameongeza kuwa taasisi hiyo pia inaendelea kuwapatia mafunzo ya uongezaji dhamani wa zao hilo kwa kuzalisha bidhaa za mafuta, sabuni, unga wa zao hilo na bidhaa zingine. Ameeleza kuwa lengo la mafunzo hayo ni uboreshaji wa bei ya zao hilo kwa kuuza bidhaa na kuachana na uuzaji wa mwani ghafi wenye bei ndogo.

Awali akiwasilisha taarifa ya Uvuvi ya Mkoa wa Lindi, Afisa Uvuvi wa Mkoa Ndg. Jumbe Kawambwa amesema kuwa uzailishaji wa mwani umeongezeka kutoka tani 993,064 zenye thamani ya Tsh. 640,782,400 kwa mwaka 2020/21 hadi tani 1,608,770 zenye thamani ya Tsh. 927,066,508 kwa mwaka 2021/22.

Ndg. Kawambwa ameongeza kuwa ongezeko hilo la uzalishaji limetokana na pembejeo za Kilimo cha mwani zilizotolewa kwa wakulima kutoka Wizara ya MIfugo na Uvuvi. Hata hivyo Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea na mchakato wa kutoa mikopo nafuu ya boti za uvuvi na pembejeo za mwani.

Aidha, Ndg. Kawambwa ametoa wito kwa wakulima wa mwani na wavuvi kujiunga kwenye vikundi na ushirika ili waweze kupata fursa za kuongeza mitaji kutoka taasisi mbalimbali za mikopo.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.