• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MHE: TELACK : WACHUKULIENI HATUA WALE WOTE AMBAO HAWAJAREJESHA MIKOPO YA HALMASHAURI

Posted on: June 5th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack ametoa maelekezo hayo Jumamosi, tarehe 03 Juni 2023 akiwa mgeni rasmi kwenye kikao Maalum cha Baraza la Madiwani cha kupitia utekelezaji wa hoja za Halmashauri ya Mtama zilizoibuliwa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali, CAG kwa mwaka 2021/2022.

Kikao hicho ambacho kilifanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Mtama ambapo katika hoja zilizoibuliwa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2021/2022,  ni pamoja na urejeshwaji mdogo wa fedha zilizokopeshwa Kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Mhe. Telack amewataka Maafisa maendeleo ya jamii kuwatafuta wanufaika wa Mikopo hiyo ambao hawajaresha na kuwachukulia hatua ikiwemo kuwafikisha Mahakamani.

Ameongeza kuwa mikopo hii haitolewi na serikali kwa ajili ya Kula, kununua vitenge, kuchezea unyago au kuongeza mke. Fedha hizi zinatolewa mahususi Kwa ajili ya kufanya uzalishaji na biashara.

Mhe. Telack amesisitiza kuwa suala la nidhamu ya fedha lazima liwe kipaumbele kwa wakopaji vinginevyo watafungwa. Ameongeza kuwa Serikali haina nia ya kumfunga mtu lakini kama watu sio waadilifu hakuna namna.

"Sisi hatuna nia ya kufunga watu lakini unapokuwa mwizi unapelekwa wapi... Lazima tutoe mifano kwa baadhi ya watu....hakuna njia nyingine kama watu sio waadilifu sio waaminifu...wewe unachukua mkopo badala ya kufanyia biashara unaenda kuchangia harusi, kununua vitenge." Amesem Mhe. Telack.

Kwa upande wake, Muhasibu Mkuu wa Halmashauri ya Mtama Ndg. Sospeter Charles Urassa, akisoma taarifa ya hoja inayohusu kutolewa kwa Mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu pasipo kuzingatia uwiano wa 4:4:2 Kwa mwaka 2021/2022, amesema kuwa kasoro hiyo ilikwisha rekebishwa na Mikopo iliyotolewa kwa makundi hayo matatu imezingatia miongozo ya Serikali. Ameongeza kuwa kwa Mikopo iliyotolewa robo ya pili ya mwaka 2022/2023 imezingatia uwiano wa 4:4:2 ambapo vikundi vya wanawake wamepatiwa mkopo wenye jumla ya Tsh. Milioni 36, vikundi vya Vijana jumla ya Tsh. Milioni 36 na watu wenye ulemavu jumla ya Tsh. Milioni 18.

Akizungumza wa Waandishi wa Habari baada ya kikao, Mkaguzi Mkuu wa Mkoa wa Lindi ndg. Deogratius Patrick Mtenga amesema kuwa kikao hiki kinafanyika maalum Kwa ajili ya kupitia taarifa ya ukaguzi ya mwaka 2021/2022 kwa kuwashirikisha Madiwani, Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa.

Ndg. Deogratius ameongeza kuwa hoja zinazoibuliwa na CAG zinalenga kuboresha mifumo ya ndani ya Halmashauri na usimamizi mzuri wa sheria za fedha zinazotolewa na serikali kwa shughuli za Halmashauri ikiwemo miradi ya maendeleo.
















Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.