• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mhe. Zambi amewataka wanalindi kuwa na imani na serikali

Posted on: June 22nd, 2017

Mhe. Zambi amewataka wanalindi kuwa na imani na serikali.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi amewataka wananchi wa Mkoa wa Lindi kuwa na imani na serikali kwani serikali inaendelea kuzifanyia kazi kero mbalimbali walizonazo.

Mhe. Zambi alisema haya katika futari aliyokuwa ameiandaa kwa kushirikiana na Export Trading Group (ETG) iliyofanyika katika makazi ya Mkuu wa Mkoa. “Katika Manispaa ya Lindi zipo kero tatu kubwa ambazi ni tatizo la maji Umeme na kukosekana kwa kivuko cha Kitunda”, alisema Mhe. Zambi.

Serikali imekuwa ikiendelea kushughulikia kero hizi ambapo kwa sasa ujenzi wa mradi wa maji Ng’apa unakwenda kwa kasi nzuri na wataalamu wamehakikisha kuwa maji yatatoka tarehe 3 Julai, 2017 kama walivyomuahidi Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. John Pombe Joseph Magufuli alipotembelea mradi tarehe 3 Machi, 2017. Mradi huu wa maji unagharimu zaidi ya bilioni 29 na unajengwa na kampuni ya Overseas Infrastructure Alliance ya nchini India.

Kuhusu mradi wa umeme, aliwaeleza kuwa serikali inaendelea kumsimamia mkandarasi ambapo kwa sasa ujenzi unakwenda vizuri na mradi utakamilika mwezi Julai, 2017. Ujenzi huu wa mradi wa umeme unaojengwa na kampuni ya Electrical Transmission and Distribution Company (ETDCO) ya hapa nchini kwa gharama ya shilingi bilioni 16. Mpaka sasa ujenzi wa njia kubwa ya umeme kutoka Mtwara mpaka Maumbika kwenye kituo cha kupoozea umeme imekamilika hivyo wanaendelea kukamilisha kazi zilizobakia.

Aidha, Mhe. Zambi aliwaleza kuwa kazi ya ujenzi wa maegesho kwa ajili ya kivuko cha Kitunda unakwenda vizuri. Mkataba wa ujenzi huo unaishia Novemba, 2017 na utagharimu shilingi bilioni 1.9 ambapo Mkandarasi amemuhakikishia kuwa atakamilisha kazi wa wakati. Kivuko kitakachotumika tayari kimeshatengwa na serikali hivyo maengesho yakikamilika kitaletwa.

Pia aliwaeleza ETG kuhakikisha wananunua mazao ya wakulima kwa bei halali na sio kuwanyonya wakulima kwa kununua mazao kwa bei ya chini. Amewataka wao wenyewe kusimamia ununuzi badala ya kuwategemea watu wa kati ambao husababisha mkulima kunyonywa.

Vilevile aliwatakia waislamu wote funga njema katika siku zilizobaki huku akiwasihi kuendelea kuyaishi maisha mema hata baada ya mfungo wa Ramadhan kumalizika. Pia aliwaomba wananchi kuendelea kuwaombea viongozi na taifa kwa ujumla ili nchi iendelee kuwa na amani na utulivu.

Bi Fatma Ally ambaye ni meneja mahusiano toka EGT alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kukubali kushirikiana na nao katika kuandaa futari. “ETG imeamua kuungana na Mkoa na Wilaya kufuturisha ikiwa inaadhimisha miaka 50 ya uwepo wake” alisema Bi Fatma. Pia alisema kuwa ETG malengo yake ni kumuunganisha mkulima mdogo na soko la dunia, huku akisisitiza wakulima kuzalisha bidhaa zilizo na ubora kwani soko la dunia halina huruma kwa bidhaa mbovu.

Sheikh wa MKoa wa Lindi, Sheikh Mshangani aliwataka waumini kuwa kitu kimoja kwani sote ni binadamu hivyo tofauti za dini zisiwe sababu ya watu kugombana. Pia ameipongeza serikali kwa kazi nzuri zinazofanyika huku akiwasihi wananchi wote kuwaombea vingozi, serikali na taifa kwa ujumla.

Katika Futuru hii walishiriki viongozi mbalimbali wa taasisi za serikali na binafsi, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa wafanyabiashara, wananchi.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.