• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MKUU WA MKOA WA LINDI AKEMEA VITENDO VYA RUSHWA KWA WATUMISHI WA SERIKALI

Posted on: November 15th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack amekemea vitendo vya rushwa katika utoaji wa huduma kwa wateja na maeneo ya kazi kwa ujumla.

Mhe. Telack amekemea vitendo hivyo viovu leo kwenye kikao cha baraza la wafanyakazi la Mkoa wa Lindi kilichofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Sea View. Akifungua kikao hicho kilichohudhuriwa na wajumbe wa baraza hilo kutoka Wilaya za Lindi, Mhe. Telack amesema kuwa vitendo vya rushwa vinarudisha nyuma maendeleo ya taasisi na taifa zima. Ameongeza kuwa wafanyakazi wa Serikali wanapaswa kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni na taratibu za utumishi wa umma ikiwemo upendo, kuheshimiana na kuepuka vitendo vya rushwa.

“Mambo ambayo kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma hayapaswi ni pamoja na kutoa na kupokea rushwa, jambo hili linaturudisha nyuma sana, ukipokea rushwa ukiwa kwenye nafasi yako………..huwezi kufanya chochote kwake, umeuza utu wako, umeuza nafasi yako ya kazi, umeuza mamlaka ambayo umekabidhiwa.” Amesema Mhe. Telack.

Mhe. Telack amewataka wafanyakazi wa umma kuacha tabia zilizo kinyume na taratibu za kazi hasa rushwa ili kujenga jamii na taifa safi lisilo na rushwa.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi, Idara ya Utawala na Raslimali watu Dkt. Bora Haule amekemea wafanyakazi ambao hawazingatii maadili ya utumishi wa umma ikiwemo uvaaji mbaya, lugha mbaya, uchafu na unywaji pombe unaopelekea vitendo visivyofaa kwa jamii. Dkt. Bora pia amewataka wafanyakazi kutoa huduma bila upendeleo wa kundi lolote kama vile siasa, dini, undugu, urafiki na kusisitiza kuwa mfanyakazi ana wajibu wa kusimamia vizuri fedha na mali ya umma na ni wajibu wake kuzuia uharibifu, upotevu, ubadhilifu wa raslimali hizo.

Akisoma taarifa ya Baraza la Wafanyakazi, Katibu wa baraza hilo Mkoa wa Lindi ndg. Jumbe Kawambwa akiipongeza Serikali ya Rais. Samia Suluhu Hassan kwa kutatua changamoto nyingi za wafanyakazi wa serikali ikiwemo malipo ya malimbikizo ya madeni, upandaji wa vyeo, mishahara kutoka kwa wakati na mengine mengi ameahidi kufanya kazi kwa weledi, unyenyekevu na kujituma katika kuwasaidia wananchi na kufikia malengo ya Serikali.

Kikao cha Baraza la Wafanyakazi kimefanyika leo ili kujadili na kufanya tathmini ya utekelezaji wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022 na mpaka kufikia Oktoba ya mwaka mpya 2022/2023.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.