• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MSF KUBORESHA HUDUMA ZA MAMA NA MTOTO LIWALE- LINDI

Posted on: August 16th, 2022

 Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Mh. Ngusa Dismas Samike leo tarehe 16/8/2022 amesaini hati ya  makubaliano  ya mradi wa  Mama na Mtoto Kwanza utakaosimamiwa na shirika la madaktari wasio na mipaka (MSF) ambao utafanyika katika wilaya ya Liwale, mkoani Lindi.

Awali, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi,Dokta. Kheri  Kagya ameeleza kuwa mradi huo umelenga kuongeza na kuboresha huduma za mama na mtoto katika wilaya ya Liwale “Mradi huu unaenda kufanya kazi katika eneo la mama na mtoto ambapo tumekusudia kuboresha huduma za afya ya uzazi ili kupunguza vifo vya akinamama na watoto wachanga wakati wa kujifungua, tutapata wasaa wa kubadilishana na kupeana uzoefu yaani capacity building, lakini pia wafadhili wetu watatupatia nguvukazi watu ambapo tunategemea mradi huu utaajiri watumishi  41 ambao ili tu tuweze kuboresha huduma zetu na afya ya mama na mtoto na ndio msingi wa mradi huu wa Mama na Mtoto Kwanza”

Naye, Kiongozi wa MSF nchini ndg. Hassan Mieki  amesema kuwa walifanya tafiti mbalimbali katika kubaini ni wilaya gani ina uhitaji zaidi wa huduma bora za mama na mtoto katika mkoa wa Lindi ambapo baada ya tafiti wakabaini kuwa uhitaji mkubwa upo katika wilaya ya liwale licha ya kuwepo kwa changamoto katika wilaya nyinginezo.

“Tunaamini ya kuwa mradi huu hautakuwa wa mwisho katika mkoa huu bado tutaendelea na miradi mingine kama njia ya kuona ni kwa namna gani tutaendelea kuboresha huduma za afya ili tuweze kusaidia jamii zetu katika sekta hii ya afya.” Ameongeza .

Aidha, mhe. Ngusa Samike, Katibu Tawala mkoa wa Lindi, amesema kuwa huduma za afya hasa afya ya mama na mtoto ni jambo ambalo halina mjadala na la umuhimu.

“Afya ya mama na mtoto ni jambo la umuhimu na halina mbadala, inasikitisha kuona mama anafariki wakati anajifungua hivyo inaleta faraja kuona na mashirika pia mnaunga mkono harakati za serikali katika kuboresha huduma hizi za afya, lakini pia tunavyofurahia kuletwa kwa miradi pia tujitahidi kuboresha, kusimamia huduma na utekelezaji wa miradi husika kwani tunaposhindwa kusimamia utekelezaji wa miradi hii kwa wakati tunakwamisha na kuchelewesha upatikanaji wa huduma za afya kwetu wenyewe na wananchi. Ameongeza.

Mradi wa Mama na Mtoto Kwanza unatarajiwa kutekelezwa katika zahanati 4, vituo vya afya 2 na hospitali ya wilaya 1 vyote ndani ya wilaya ya Liwale.

 

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.