• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MWENGE WA UHURU WAANZA KUKIMBIZWA MKOANI LINDI HUKU MRADI MMOJA UKIKATALIWA

Posted on: July 4th, 2021

Mwenge wa Uhuru umepokelewa Mkoani Lindi leo tarehe 23 Agosti 2021 kutoka Mkoa wa Dar es salaam baada ya kumulika miradi mbalimbali ya Mkoa huo. Akiupokea Mwenge na timu ya wakimbiza Mwenge kitaifa wakiongozwa na Luteni. Josephine Mwambashi, Mhe. Zainab R. Telack amemueleza Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mhe. Amosi Makala kuwa Mwenge utakimbizwa takribani km 815.8 Mkoani Lindi kwa kudumisha amani, upendo na mshikamano ambapo utamulika miradi 42 mkoa mzima.

Kiongozi wa mbio za Mwenge Luteni. Josephine Mwambashi aliwaeleza viongozi wa Mkoa na Wilaya kuwa katika miradi yote inayomulikwa na Mwenge wahakikishe nyaraka na taarifa zote za mradi  husika zinakuwepo eneo la mradi, wahusika wa mradi wawe na uwezo wa kujieleza na kujibu maswali. Pamoja na maelekezo hayo kiongozi huyo alisisitiza kuchukua hatua zote za kujikinga na ugonjwa wa UVIKO-19 ikiwemo uvaaji wa barakoa, kunawa kwa vitakasa mikono na kujitokeza kuchoma chanjo.

Aidha, baada ya makabidhiano ya Kimkoa, Mhe. Zainab R. Telack alimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Zainab Rashid Kawawa tayari kwa kuanza mbio hizo kumulika miradi ya Wilaya hiyo.

Baada ya kukabidhiwa Wilaya ya Kilwa, Mwenge ulifanikiwa kutembelea zaidi ya 11 ambayo ni mradi wa kituo cha afya Somanga pamoja na mifumo ya TEHAMA ya kituo hicho, mradi wa maji wa Somanga, Shamba la korosho ekari 50 la mkulima ndg. Hussein Yusuph, Klabu ya kupambana na rushwa na Klabu ya lishe za wanafunzi wa Shule ya Sekondari Ilulu, mradi wa mashine ya kusaga ya watu wenye ulemavu kijiji cha Matandu, mradi wa kiwanda cha maji safi ya kunywa kilichopo Nangurukuru, mradi wa barabara ya kivinje yenye km 4.2, programu za mapambano dhidi ya malaria, madawa ya kulevya na UKIMWI Hospitali ya Kinyonga-Kilwa Kivinje na mwisho ni mradi wa usarishaji wa Kilwa jogging club.  

Katika miradi yote iliyotembelewa na Mwenge, kiongozi wa mbio za Mwenge alikataa kuzindua mradi wa maji wa Somanga kutokana na kiasi cha fedha kilichotumia kutoakisi uhalisia wa mradi huo. Kiongozi huyo alisema “ mradi umekamilika lakini nyumba ndogo ya mtambo wa maji haiwezi kujengwa kwa Tsh. Milioni 26 na tenki milioni 150, hakuna uhalisia, fedha zimetumika nyingi ukilinganisha na mradi wenyewe.” Alisisitiza watendaji kutekeleza na kusimamia miradi kwa uzalendo na kisha aliagiza TAKUKURU kufanya uchunguzi wa mradi huo.

Mwenge wa Uhuru unaendelea kukagua miradi ya Wilaya za Mkoa wa Lindi ukiwa na kauli mbiu “TEHAMA NI MSINGI WA TAIFA ENDELEVU; ITUMIE KWA USAHIHI NA UWAJIBIKAJI” ambapo utahitishwa na kukabidhiwa Mkoa wa Mtwara tarehe 28 Agosti 2021.       

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.