• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Nachingwea yapewa pongezi

Posted on: April 8th, 2020

Nachingwea yapewa pongezi

Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea yapongezwa kwa kutoa mafunzo kwa vikundi kazi vya wanawake na vijana kuhusu utengenezaji wa barabara.

Akizungumza kabla ya kuwakabidhi vyeti wahitikimu wa mafunzo hayo Mkuu wa mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi ameupongeza uongozi wa wilaya ya Nachingwea na halmashauri kwa kuratibu mafunzo hayo. Pia amekipongeza chuo cha teknolojia stahiki ya nguvu kazi (ATTI) kwa kukubali kwenda Nachingwea na kutoa mafunzo kwa vikundi hivyo. Vilevile amewapongeza wanakikundi kwa utayari wao wa kupata mafunzo.

Zambi amewataka mameneja wa TARURA mkoa wa Lindi kuvitumia vikundi hivi hasa pale wanapokuwa na kazi ndogondogo za ukarabati na matengenezo ya barabara kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kuongeza ajira na uchumi kwa wananchi.

Wanavikundi wametakiwa kuhakikisha kazi watakazopata wanazifanya kwa weledi mkubwa na kutumia maarifa yote waliyopatiwa ili kuhakikisha ubora unaotakiwa unafikiwa. Zambi amesema iliyotengenezwa wakati wa mafunzo ni ya ubora sahihi ambayo mtu hawezikujua kama imetengenezwa kwa kutumia nguvu kazi na sio mitambo mikubwa.

Akizungumzia mafunzo hayo, mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Hassan Rugwa amesema halmashauri imetoa mikopo kwa vikundi kazi 15 ambavyo vimepatiwa mafunzo hayo na wakufunzi kutoka chuo cha teknolojia stahiki ya nguvu kazi (ATTI) kilichopo Tukuyu – Mbeya. Pia vipo vikundi 4 ambavyo vimejigharamia kushiriki kwenye mafunzo kutokana na kutokidhi vigezo vya kupata mkopo.

Vikundi hivi vimepatiwa mkopo wa milioni mbili kila kikundi ambazo zimetumika kugharamia mafunzo hayo na ununuzi wa vifaa anzia vya kazi (matoroli, masepetu, nyundo, sururu, majembe, shoka, tape measure pamoja na kufungulia ofisi zao za ukandarasi.

Rugwa ametaja faida ambazo vikundi hivyo vitazipata ikiwemo ya upataji ujuzi wa ukarabati na utengenezaji wa barabara kwa kutumia teknolojia stahiki ya nguvu kazi, vikundi vinaweza kupata kazi za ukarabati na matengenezo ya barabara kupitia TARURA na TANROAD, na vikundi hivi vinakwenda kutambuliwa na bodi ya wakandarasi kwani vitapata vyeti vya BRELA na CRB.

Donata Amlima (mwanakikundi) ameishukuru halmashauri kwa kuwawezesha kupata mafunzo. Lakini ameiomba halmashari kuwasaidia kupata kazi hizo za barabara kwani hapo ndio watapata faida ya mafunzo na sio kuwategemea wakandarasi peke yake.

Naye Faki Chilumba (mwanakikundi) amesema licha ya kufanya kazi kwenye kampuni za ujenzi wa barabara, mafunzo hayo yamemjengea uwezo mkubwa kwani kuna mambo mengi ya kitaalam ambayo alikuwa hayajui. Pia elimu hiyo ataitumia katika kijiji chake pale watakapokuwa wanataka kutengeneza au kufungua barabara.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Mhe. Ahamad Makoroganya amesema madiwani walitumia busara kubwa kubadilisha njia ya uwezeshaji vikundi ambayo ni ya kuvipatia elimu ya utaalam itakayo wapa ujuzi wa kufanya kazi badala ya kutoa kwa vikundi vya wajasiriamali peke yake. Halmashauri itakuwa ikivitumia vikundi hivi kwenye kazi za ufunguaji barabara.

Mkufunzi wa kutoka chuo cha ATTI, Mhandisi. Paul Henry amesema mafunzo hayo yanalenga kuviimarisha vikundi ili viweze kufanya kazi hizo katika ngazi za chini badala ya kuwategemea wakandarasi ambao huwa na gharama kubwa. Lakini pia hutolewa kwa wataalam wa ujenzi kutoka ngazi/idara mbalimbali zikiwemo TANROADS na TARURA.

Mhandisi. Henry amesema anaimani kuwa wahitimu wote watakwenda kufanya kazi kwa kuzingatia mafunzo waliyowapatia na itakuwa ni mwanzo wa barabara nyingi katika ngazi za vijiji na kata kufunguka.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.