• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Ngubiagai: Wananchi pandeni miti

Posted on: April 26th, 2019

Ngubiagai: Wananchi pandeni miti

Wananchi wametakiwa kupanda miti na kuitunza ili kusaidia utunzaji wa mazingira na kujiletea maendeleo.

Hayo yamesemwa na mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Lindi ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mhe. Christopher Ngubiagai wakati akizungumza na wananchi kwenye maadhimisho ya siku ya upandaji miti iliyofanyika kimkoa wilayani Kilwa.

Ngubiagai amesema wananchi wanao wajibu mkubwa wa kuhakikisha wanapanda miti ya aina mbalimbali katika maeneo yaliyotengwa kwa kazi hiyo ikiwa ni pamoja na upandaji wa miti ya matunda katika makazi yao.

Pia ameziagiza halmashauri kuhakikisha zinafanya mapitio ya hali ya miti iliyopandwa miaka ya nyuma ili kujua ni miti kiasi gani imekua, kwani kumekuwepo na tatizo la kutokuwa na ufuatiliaji wa ukuaji wa miti inayopandwa kila mwaka.

“Niziagize halmashauri zote katika mkoa wa Lindi kuhakikisha zinatenga maeneo kwa ajili ya upandaji miti na kupanda miti, pia kuhakikisha zinawahamasisha wananchi kupanda miti ya matunda katika maeneo yao”, alisema Ngubiagai.

Aidha, amewasihi wananchi kuendelea kutumia misitu katika kujiletea maendeleo kwa ufugaji nyuki na uvunaji endelevu wa misitu. Pia amezielekeza halmashauri kuendelea kuvisaidia vijiji ili viweze kuwa na mpango wa matumizi bora ya ardhi ambapo itaviwezesha vijiji kuwa na mpango wa uvunaji endelevu wa misitu.

Akitoa salamu kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu, Dkt. Bora Haule alisema pamoja na kutenga maeneo ya kupanda miti ni vizuri pia kwa Halmashauri wakajiwekea utaratibu wa kuandaa kazu data ya miti iliyopo katika maeneo yao.

Awali akisoma taarifa ya miti ya mkoa Afisa Maliasili Mkoa, Zawadi Jilala alisema kuwa  ili kuhakikisha shughuli za usimamizi shirikishi za misitu zinakuwa endelevu, Mkoa wa Lindi kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii imeanzisha programu ya uongezaji wa thamani wa mazao ya misitu na nyuki unaofadhiliwa na serikali ya Finland.

Mkoa wa Lindi umeweka malengo ya kupanda miti mchanganyiko 15,000 kwa kila wilaya.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.