• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

RAS SAMIKE: WASIMAMIZI WA MIRADI KILWA ACHENI VISINGIZIO.

Posted on: September 1st, 2022

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa wametakiwa kuacha visingizio na badala yake waongeze kasi ya usimamizi na utekelezaji wa miradi mbalimbali ili kurahisisha upatikanaji wa huduma hasa za afya kwa wananchi.

Maagizo hayo yametolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Ngusa Samike  wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya afya na elimu katika wilaya ya Kilwa ambapo amebaini uzembe unaofanyika na watumishi hao katika usimamizi wa mradi wa ujenzi wa kituo cha afya uliopo katika kijiji cha Kipindimbi.

Akitoa taarifa ya mradi bi. Emiliana Mlelwa, mganga mfawidhi wa zahanati ya Kipindimbi amesema “Mradi wa kituo cha afya Kipindimbi unagharimu kiasi cha shilingi Milioni 500,na ulichelewa kutekelezwa kutokana na mgogoro ulioibuka katika kijiji cha Njinjo kwa kudai kuwa kituo kinapaswa kujengwa Njinjo badala ya Kipindimbi, hivyo mradi ulianza kutekelezwa tarehe 16/01/2021 baada ya kupokea maelekezo kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa na ulitarajiwa kukamilika tarehe 17/04/2022, lakini pia tumekuwa na changamoto ya kufungwa kwa mfumo wa malipo na kupelekea mafundi kutokuwepo site pamoja na wazabuni kuchelewesha vifaa”  

 Katika kuhakikisha mradi huo unakamilika Katibu Tawala amewataka wasimamizi wa ujenzi huo kuacha visingizio na kuhakikisha mradi huo unakamilika “wasimamizi wa huu mradi hasa ambao ni watumishi tuache visingizio kama vile uwepo wa mvua au kufungwa kwa mfumo wa malipo kama sababu ya mradi kutokukamilika, tukubali tu kuwa kuna uzembe katika usimamizi,naagiza mradi kuendelea na ujenzi kuanzia kesho, mkurugenzi naomba uhakikishe mafundi wanakua site huku taratibu za kukagua thamani za mradi zikifuata”

Aidha, amemtaka mganga mkuu wa wilaya ya kilwa kuanza taratibu za kuomba watumishi, madawa na vifaa tiba ili punde mradi utakapokamilika uanze kutoa huduma kwa wananchi.

Mradi wa kituo cha afya Kipindimbi unajumuisha majengo matano ambayo ni jengo la wagonjwa wa nje (OPD), jengo la maabara, jengo la kufulia, jengo la upasuaji na jengo la wodi ya wazazi, pia unatarajiwa kuhudumia wananchi wapatao 30,861 wa kata ya Njinjo pamoja na wakazi wa kata jirani za Miguruwe, Kandawale na Mitole.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.