• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

RC TELACK ATAKA ELIMU YA LISHE ITOLEWE KWA JAMII

Posted on: November 9th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack amewataka Waganga Wakuu wa Hospitali za Wilaya kutoa elimu ya lishe kwa jamii ili kupata kizazi chenye uwezo wa kufanya maamuzi sahihi. Mhe. Telack ameyasema hayo kwenye kikao cha kusaini mikataba ya utekelezaji masuala ya lishe kati ya Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa.

Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika jumanne katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa na kuhudhuriwa na Kamati za Usalama, kamati za lishe za Mkoa, Wilaya pamoja na wafadhili wakuu Save The Children, Mhe. Telack akisisitiza utoaji wa elimu amesema kuwa lishe duni ndiyo chanzo cha matatizo yanayotokea kwenye jamii ikiwemo kupigana hovyo.

“Sote tunajua kwamba tukisimamia lishe tutakuwa na watu wenye maamuzi…sio tunazaa watoto wanapiga wenzao mikuki……ukiangalia utakuta kuna matatizo kwenye kichwa…….tusaidiane kujenga nchi yetu, tusaidiane kujenga watoto wetu.”

“Elimu ya lishe itolewe kwenye vituo vyote vya kutolea huduma kabla kina mama hawajapima ujauzito, lakini kabla watoto hawajapimwa, wazazi wanahitaji kupatiwa elimu….mwingine anampa mtoto wake kile anachokiona na hajui madhara yake ili mradi mtoto ashibe, sasa wataalam tusaidieni…..kwenye vituo vya afya tukawe na orodha ya vyakula vya lishe bora…..wazazi wafundishwe.”

Kwa upande wake Mratibu wa Lishe Mkoa wa Lindi Ndg. Lewis Mahembe amesema kuwa kwa sasa Mkoa wa Lindi unapiga hatua nzuri kwenye uboreshaji wa lishe kwa jamii ambapo kwa takwimu za mwaka jana Mkoa wa Lindi ulikuwa wa tatu kutoka mwisho na mwaka huu mkoa umeshika namba 10 kitaifa. Ndg. Lewis ameongeza kuwa changamoto kubwa kwenye utekelezaji mpango wa lishe ni matumizi ya fedha zilizopangwa kuboresha lishe kutumika kinyume na mpango huo.

Katibu Tawala Mkoa wa Lindi Ndg. Ngusa Samike amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Lindi kutumia fedha za lishe kama inavyoelekezwa na Serikali ili kufikia malengo yaliokusudiwa. Ndg. Ngusa pia amewataka Waganga Wakuu wa Wilaya pamoja na Maafisa Lishe kuwajibika ipasavyo katika kuboresha afya ya mama na mtoto.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.