• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

REA YAFANYA TATHMINI YA MIRADI YA UMEME VIJIJINI, MKOA WA LINDI

Posted on: January 27th, 2023

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi wamefanya kikao na wadau leo tarehe 27 Januari, 2023 chenye lengo la kujadili maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya REA kwa awamu ya Tatu mzunguko wa Pili katika mkoa wa Lindi ambao umeganywa kwa wakandarasi wawili, Nakuroi Investment Company Limited (Lot 10) na White City International Contractors LTD (Lot 11).

Mhandisi Thomas Mbaga, Kaimu Mkurugenzi Mkuu REA ameeleza kuwa mradi wa REA awamu ya Tatu, mzunguko wa Pili kwa mkoa wa Lindi unagharimu kiasi cha shilingi za kitanzania Bilioni 71.915 na unatekelezwa katika wilaya za Kilwa, Lindi Vijijini (Mtama), Ruangwa, Nachingwea na Liwale ambapo mikataba yake ilisainiwa mnamo Juni 2021 na kutegemewa kukamilika ndani ya muda wa miezi 18.

“Lengo letu ni kuhakikisha kuwa vijiji vyote vilivyopo Tanzania Bara vinafikiwa na miundimbinu ya umeme, na huu ndo mradi wa kufunga mambo yote ya kupeleka umeme katika vijiji vyote vya Tanzania Bara. Katika mkoa wa Lindi vijiji 198 vipo katika utekelezaji wa mradi wa mradi huu wa REA Three, Phase two ambapo Nakuroi Investment yeye anapeleka umeme katika vijiji 92 vya wilaya ya Kilwa, Lindi vijijini pamoja na Ruangwa. Na Mkandarasi White City anapeleka umeme katika vijiji 107 ambavyo vipo katika wilaya za Nachingwea(70) na Liwale(37)”

Mhandisi Mbaga ameongeza kuwa katika utekelezaji wa mradi huo katika maeneo mbalimbali kumejitokeza changamoto kadha wa kadha ambazo zimechochea kudhorotesha ufanisi wa utekelezaji wa mradi huo katika maeneo ya miradi

“Kulitokea na ongezeko ambalo si la kawaida la vifaa ikiwemo nyaya kwahoiyo ongezeko hilo lilisababisha tukae chini na kujadili ni kwa namna gani tunaweza kulitatua na tunashukuru tumeweza kulipatia utatuzi na tumeshaona ni sehemu gani tunaweza kuboost ili zoezi hili lisikwame, lakini pia tulipata changamoto za wizi wa vifaa na uwepo wa baadhi ya vijiji katika Pori la Akiba la Selous hivyo kuhitajika vibali vya serikali ili kuemdelea na shughuli hizo”

Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Ndg. Ngusa Samike  amewataka wakandarasi kuacha visingizio na kujitahidi kumaliza kazi kwa wakati uliowekwa ili kuisahidia serikali kufikisha huduma kwa wakati sahihi kwa wananchi na kwa ubora unaotakiwa.

“Wakandarasi mnaofanya kazi kwatika miradi iliyopo hapa Lindi tunawataka muache visingizio, mliomba kazi, mkapewa kazi, mkafanye kazi ndo ujumbe tunawapatia, na kwakua mumekuja na mnalipwa fedha za serikali ni vyema mkaenda kufanya kazi kwa mujibu wa mkataba kwanza mtekeleze mradi kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.nikifika maeneo ya mradi nategemea kumuuliza swali mkandarasi na anijibu kwa kueleweka kwasababu matarajio yrtu sisi ni wananchi wa mkoa wa Lindi wapate huduma inayostahili”

Kwa upande wa wakandarasi wameeleza kuwa mfumuko wa bei za vifaa hasa zenye asili ya chuma ndizo zilizochochea wao kushindwa kukamilisha miradi yao kwa wakati uliopangwa.

“Hadi sasa hivi tunaendelea vizuri, tulikua na baadhi ya changamoto hasa ya kuongezeka kwa bei za vifaa vyenye asili ya chuma kama nyaya bei ilipanda ikawa kubwa kubwa sana tunaishukuru serikali iliingilia kati na kutusaidia kutatua changamoto hiyo, na hivyo tunaamini katika miezi hii mitatu iliyobaki tunaweza kukamilisha kabisa kazi tulizokuwa nazo” Mhandisi Jacqueline Mushi, Meneja Miradi wa kampuni ya White City.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.