• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

SERIKALI YAENDELEA KUPAMBANA NA UKIMWI MAKAZINI

Posted on: November 22nd, 2022

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kupambana na magonjwa ya kuambukiza na yasioambukizwa mahali pa kazi. Hayo yamebainika jana katika kikao cha kamati ya kitaifa na Mkoa ya kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa sugu yasioambukizwa mahali pa kazi katika utumishi wa umma kilichofanyika Mkoani Lindi, ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Akizungumza wakati akifungua kikao hicho, Naibu Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ndg. Xavier M. Daudi amewakumbusha wajumbe wa kamati hizo za kitaifa na mkoa kuzingatia utekelezaji wa Sheria ya UKIMWI ya mwaka 2008 pamoja na Mkakati wa Nne wa kudhibiti UKIMWI 2018-2023. Ameongeza kuwa Tanzania imelenga kuhakikisha inafikia lengo la Kimataifa la 95-95-95 ifikapo 2025 yaani ikimaanisha 95% ya wanaoishi na VVU wanatambua hali zao, 95% ya WAVIU wawe wameanza dawa ya kupunguza makali ya VVU na 95% ya walioanza dawa wapunguze kiwango cha virusi mwilini.

Katika kufikia malengo hayo Ndg. Xavier M. Daudi amezielekeza wizara na mikoa kuhakikisha zinatenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Afua za VVU, UKIMWI , kuwashauri Waajiri kuhusu umuhimu wa kufanya mazoezi na kupima afya za watumishi mara kwa mara.

“Suala la mazoezi ni kitu ambacho halihitaji raslimali fedha, hivyo tujenge utamaduni wa kushirikiana na kuhamasishana kufanya mazoezi ya mara kwa mara. Utaratibu huu utapunguza changamoto nyingi za kiafya kwani mazoezi ni tiba.” Amesema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Anuai za Jamii kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Mwanaamani Juma Mtoo akizungumza na waandishi wa habari amesema kuwa Lengo la kuja Mkoani Lindi ni pamoja na kuona Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Halmashauri zake namna gani zinasimamia na kutekeleza Afua mahali pa kazi ili serikali iweze kufikia malengo yake kwa kuwa na wafanyakazi wenye afya bora. Amesema kuwa kupitia  Sera ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma ya mwaka 2008, unaandaliwa mwongozo wa namna ya kudhibiti VVU, UKIMWI na Magonjwa sugu yasioambukizwa mahali pa kazi ambao pia utatumika kudhibiti matatizo ya msongo wa mawazo na matatizo ya akili.

Akisoma taarifa ya Mkoa wa Lindi na Halmashauri zake Katika kupambana na magonjwa VVU,  UKIMWI na magonjwa yasioambukizwa Dkt. Bora Haule amesema kuwa jitihada mbalimbali zinafanyika ikiwemo utoaji wa elimu, kuhamasisha wafanyakazi kupima ili kufahamu afya zao, kusambaza kinga kwa wafanyakazi, kutoa chakula lishe, kutoa fedha kila mwezi kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa VVU.

Ikumbukwe kuwa vyanzo vikubwa vya magonjwa yanayoambukizwa na yasioambukizwa yanasababishwa kwa kiasi kikubwa na tabia zisizofaa ikiwemo ulaji usiozingatia utaratibu wa lishe bora, tabia za kutofanya mazoezi, ngono isio salama nk. Hii imesababisha kupungua kwa nguvu kazi na familiana taifa kwa ujumla hivyo kushusha uzalishaji na uchumi kwa ujumla.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.