• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

SIKU YA KOROSHO YAADHIMISHWA KWENYE MAONYESHO YA NANENANE.

Posted on: August 6th, 2022


Bodi ya Korosho Tanzania kwa kushirikiana na taasisi ya Utafiti Naliendele (TARI), jana tarehe Agosti 05,  imeadhimisha siku ya Korosho pamoja na kuzindua kampeni ya Ulaji na Utumiaji wa bidhaa zitokanazo na zao hilo ikiwemo maziwa, mvinyo na sharubati  itokanayo na Korosho kama njia ya kutoa msukumo uzalishwaji  wa zao hilo kwa wingi na kwa kuzingatia ubora na viwango vya kimataifa.

Awali Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania, amesema “Takwimu zinonyesha ubanguaji wa korosho hadi sasa ni sawa na asilimia mbili tu hivyo inakua ngumu kufikia lengo la asilimia sitini ya ubanguaji ifikapo 2024/2025 ikiwa sisi wenyewe hatutumii kile tunachozalisha kwa wingi  hivyo maadhimisho ya siku ya korosho yanafanyika ili kuhamasisha matumizi ya korosho kuanzia kwa soko la ndani ya nchi na bidhaa zake nyingine pia kuvutia zaidi wawekezaji”

Aidha, Kaimu Meneja Idara ya Uchumi Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Bwana Aristedes Mrema, amesema kuwa Benki Kuu inakitazama kilimo cha Korosho kama zao muhimu sana kwa ustawi wa nchi na ustawi wa uchumi kwa mikoa ya kusini kwani licha ya kuongeza kipato kwa mwananchi mmoja mmoja katika ukanda huu pia ni moja ya zao la kimkakati linaloiingizia nchi fedha za kigeni.

“Kiasi cha Korosho kinachobanguliwa hapa nchini ni takribani ya asilimia kumi tu ya korosho zote zinazopatikana hapa nchini kwa mwaka, jambo hili linaipotezea nchi fedha nyingi sana hivyo juhudi kama hizi za kuipa thamani korosho hapahapa nchini ni jambo lenye manufaa kwa nchi kiuchumi na kijamii pia.” Ameongeza Mrema.

Kanali Ahmed Abbas, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye ndiye Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ya Siku ya Korosho yaliyofanyika katika viwanja vya maonyesho ya Nanenane kwa kanda ya Kusini, Ngongo, ameipongeza Bodi ya Korosho na Taasisi ya Utafiti Naliendele (TARI) kwa tafiti mbalimbali wanazozifanya zenye tija kwenye mazao mbalimbali ya kilimo ikiwemo zao la Korosho.

“Kiupekee niwapongeze sana Bodi ya Korosho na TARI Naliendele kwa kuandaa na kuazimisha siku hii ya Korosho na kupitia tafiti hizi zilizofanywa zitokanazo na korosho hapa tumepata mvinyo, maziwa ambayo yanatokana na Korosho,na  utaratibu huu utachochea sana kukua kwa sekta ya ujasiriamali na katika namna ya pekee sana utaongeza na kuchochea mnyororo wa thamani wa zao la Korosho” amesema Kanali Abbas.

 


Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.