• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

SIKU YA MACHO DUNIANI: WANANCHI NA WANAFUNZI WAHIMIZWA KUZINGATIA AFYA NA USALAMA WA MACHO YAO

Posted on: October 10th, 2024

Katika kuadhimisha siku ya macho duniani, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi Sokoine kwa kushirikiana na Shirika la Heart to Heart Foundation, Korean Church na CBM wamewafikia wananchi wapatao 10,378 mkoani Lindi  kwa kuwapa huduma ya elimu ya afya ya macho huku kati yao 9690 wamefanyiwa vipimo na kupatiwa matibabu kupitia kambi mbalimbali zilizoendeshwa katika wilaya zote za Mkoa wa Lindi.


Akizungumza kwa niaba ya Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Sokoine Dkt. Sharifu Hamza ameeleza kuwa zoezi hilo lililoendeshwa kwa siku saba kuanzia oktoba 4 hadi 7 wataalamu walipita katika shule mbalimbali za halmashauri zote sita kutoa elimu pamoja na kutoa matibabu kwa wananchi na wanafunzi walioonekana na changamoto ya afya ya macho na kuongeza kuwa imekua ni faraja kwa wananchi kusogezewa huduma bora za macho hivyo zoezi hilo limekuwa na mafanikio makubwa.


Bwana. Edward Aloyce Afisa mradi kutoka shirika la Heart to Heart Foundation amesema shirika lao limekuwa likifanya mradi wa macho katika Mkoa wa Lindi na kuongeza kuwa katika kambi ya mwaka huu wamelenga kupata watoto 20 wenye changamoto ya mtoto wa jicho ambao watanufaika kwa kupata huduma ya operesheni bure.


"Tumesukumwa kwa sababu watoto ndio wanapata changamoto kubwa katika tatizo la macho na tumefanya kwa ushirikiano pamoja na hospitali hii ya Lindi Sokoine lakini pia tutafanya na hospitali ya taifa ya muhimbili kwa kuleta madaktari bingwa baada ya watoto hao kuweza kuhainishwa kutokana na changamoto zao za magonjwa ya macho"


Hata hivyo, Aloyce ametoa wito kwa wananchi, wazazi na watoto kujenga tabia kufanya uchunguzi wa changamoto za macho katika hospitali ili kujikinga na maradhi mbalimbali ya macho yanayoweza kuleta athari kubwa ikiwemo upofu. 


Dokta. Mwacha Machaja, Mtaalamu wa huduma za macho Mkoa na Hospital ya Rufaa ya Lindi Sokoine amesema zipo sababu mbalimbali zinazopelekea matatizo ya macho ambapo miongoni kwa sababu hizo ni umri, ajali, lishe duni , maambukizi  na sababu za  kuzaliwa.


"Wakazi wengi wa Lindi wanaopata changamoto ya macho inatokana na kutokula vyakula vinavyolinda macho hususani kuimarisha ukuta wa jicho na mishipa ya fahamu ikiemo mboga za majani ambazo hazijapikwa sana kiasi cha kupoteza rangi yake pamoja na karoti iliyopikwa"amefafanua.


Siku ya Macho Duniani huadhimishwa kila mwaka ifikapo Oktoba 10 ambapo kwa mwaka huu maadhimisho hayo yamepambwa na kauli mbiu isemayo 'Penda Macho Yako, Muhamasishe Mtoto Kupenda Macho Yake' imelebga zaidi kuhamasisha watoto na wanafunzi kupenda na kujari afya ya macho kwa kuwapa elimu mbalimbali juu ya afya ya macho na namnq ya kujikinga dhidi ya maradhi ya macho. 

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.