• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

TAKUKURU KUCHUNGUZA MRADI WA UJENZI WA BWENI

Posted on: April 14th, 2023

Taasisi ya kupambana na rushwa, PCCB Wilaya ya Kilwa imeagizwa kufanya uchunguzi wa fedha na maendeleo yasioridhisha ya ujenzi wa bweni la watoto wenye mahitaji maalum unaendelea katika Shule ya Msingi Mtanga iliyopo Kilwa Masoko, Wilayani Kilwa kwa fedha za Maadhisho ya Uhuru wa Tanzania bara ya mwaka 2022.

Maagizo hayo yametolewa Leo tarehe 14 Aprili 2023 na kiongozi wa Mwenge wa Uhuru ndg. Abdalla Shaib Kaim baada ya Mwenge wa Uhuru kutembelea na kukagua mradi huo ulioanza kujengwa tarehe 05 Februari 2023.

Akiweka jiwe la msingi kwenye mradi huo, ndg. Kaim amesema kuwa kutokana na ukaguzi uliofanyika zimebainika changamoto zinazohusu mradi ikiwemo kwenye ghala la kuhifadhia bidhaa za ujenzi wa mradi.

Ndg. Kaim amekili kutokuwa na mashaka juu ya ubora wa mradi, kuwa ni wa kuridhisha lakini changamoto kubwa ni mradi kuchelewa kumalizika kwa wakati. Ameongeza kuwa mradi umechelewa kumalizika lakini wataalam hawana majibu yanayotosheleza ni kwa nini mradi haumaliziki.

Aidha, Ndg. Kaim ameongeza kuwa watoto wenye mahitaji maalum wanahitaji kuyatumia mabweni mapya kwa mahitaji yao ambayo yatawapa fursa ya kupata elimu bora.

Awali akisoma taarifa ya mradi huo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mtanga Omary Mohamed amesema kuwa fedha za mradi wa bweni zilipatikana baada ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan kufanya maamuzi ya kubadilisha matumizi ya fedha za Maadhimisho ya Sherehe za Uhuru yaliyotakiwa kufanyika mwaka 2022.

Baada ya mabadiliko hayo, Shule ya Msingi Mtanga ilipatiwa jumla ya Tsh. Milioni 110 mwezi Disemba 2022 kwa ajili ya ujenzi wa bweni lenye uwezo wa kuchukua jumla ya watoto 80 wenye mahitaji maalum likiwa na vyumba 20, matundu ya vyoo 5, mabafu 5.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Christopher Ngubiagai amemshukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha ujenzi wa miundombinu rafiki itakayowasaidia watoto wenye mahitaji maalum kupata fursa ya elimu katika mazingira rafiki.



Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.