• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Tatizo la umeme na maji kumalizika Julai, 2017

Posted on: June 21st, 2017

Tatizo la Umeme na Maji kumalizika Julai, 2017

Wakandarasi wanaojenga miradi ya maji na umeme katika Manispaa ya Lindi kwa pamoja wamemuhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi kuwa miradi hiyo itakamilika ndani ya Julai, 2017.

Wakandarasi waliyasema kwa nyakati tofauti wakati Mhe. Zambi alipotembelea miradi hii. Wakati akiwa katika mradi wa maji wa Ng’apa Mhe. Zambi aliridhishwa na kasi ya ujenzi inayoendelea na kumtaka Mkandarasi huyo kukamilisha kazi kwa wakati. Ujenzi wa mradi wa maji wa Ng’apa unagharimu shilingi bilioni 29 na unajengwa na kampuni ya Overseas Infrastructure Alliance ya nchini India.

Pia Mhe. Zambi alitembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha kupoozea umeme cha Maumbika ambapo mkandarasi alimueleza kuwa ujenzi wa njia kuu ya umeme kutoka Mtwara mpaka Maumbika umekamilika. Aidha, alieleza kuwa ujenzi wa miundombinu katika kituo unakwenda vizuri na wanauhakika kuwa ndani ya Julai, 2017 tatizo la umeme litakuwa limekwisha. Mradi huu unagharimu shilingi bilioni 16 na unajengwa na kampuni ya Electrical Transmission and Distribution Company (ETDCO).

“Tatizo la kukatika kwa umeme limekuwa ni kero kubwa kwa wananchi wa Lindi, hivyo ni imani yangu kuwa mtaifanya kazi hii kwa umakini ili mradi utakapokamilika tatizo hili lisijirudi kabisa”, alisema Mhe. Zambi.

Vilevile Mhe. Zambi alitembelea mradi wa ujenzi wa maegesho ya kivuko cha Kitunda ambapo alikuta kazi ya ujenzi ikiwa inaendelea vizuri. Kampuni inayojenga mradi huu ni M/S Hematech Investment Ltd, Ira General Enterprises Co. Ltd JV na inajenga kwa gharama ya shilingi bilioni 1.9. Mradi huu unatakiwa kukamilika mwenzi Novemba, 2017 ambapo mkandarasi alimuhakikishia Mkuu wa Mko kuwa mradi utakamilika kwa wakati.

Baada ya kutembelea miradi yote hii, Mhe. Zambi aliwataka wanalindi kuwa na imani na serikali yao kwani inazifanyia kazi kero zao. Pia alisema kuwa serikali inaleta fedha nyingi Lindi kwa ajili ya maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na kushughulikia kero za wananchi ambapo alitoa mfano mdogo tu wa jumla ya fedha zinazotumika kutekeleza miradi hii mitatu.

Aidha, Mhe. Zambi aliwaomba wananchi kuendelea kushirikiana na serikali katika kujiletea maendeleo na katika kutafuta ufumbuzi wa kero mbalimbali zinazowakabili.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.