• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Tutumie maghala mkuu kudhibiti upotevu wa mazao - RC Zambi

Posted on: September 13th, 2019

Tutumie maghala makuu kudhibiti upotevu wa mazao - RC Zambi

Mkuu wa mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi amewataka viongozi na wadau wa ufuta kufikiria kutumia kutumia maghala makuu ili kudhibiti upotevu wa zao hilo.

Zambi ameyasema hayo katika kikao cha tathmini ya ununuzi wa zao la la ufuta ambapo taaarifa imeonyesha kuwepo na upotevi/wizi wa ufuta kwenye baadhi ya maghala ya vyama vya ushirika vya msingi na kusababisha wakulima kutolipwa fedha zao kwa wakati.

Katika taarifa iliyowasilishwa na mrajisi msaidizi wa mkoa, Ndg. Robert Nsunza imeonyesha kuwa upotevu huu umesababishwa na baadhi ya makarani na viongozi wa AMCOS kupoteza mizigo mfano vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) ya Nanjilinji imepoteza tani 81 za ufuta na viongozi wake kusingizia wameibiwa na chama kikuu, jambo ambalo sio la kweli kutokana na taarifa iliyotolewa na kamati ya uchunguzi iliyoundwa. Uzidishwaji wa mizigo kwa makampuni ambapo kampuni ya Hashim and SONs imezidisha tani 32 za ufuta kutoka wilaya ya Kilwa. Pia utoroshwaji wa mizigo bila kulipiwa ushuru.

Nsunza alisema kuwa tayari hatua mbalimbali zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kuunda kamati za uchunguzi, kuwafikisha katika vyombo vya usalama viongozi waliohusika na upotevu huo, na kwa kampuni zilizozidisha mzigo na ambazo zimekiri kosa hilo wamelipia fedha za mizigo hiyo. Pia mikakati ya kuhakikisha wanunuzi wanalipia na ushuru wa halmashauri kulingana na kiasi cha mzigo waliozidisha imefanyika.

Nae Mkuu wa wilaya ya Nachingwea. Mhe. Rukia Muwango amelalamikia kitendo cha baadhi ya wazabuni kuchelewa kuchukua mizigo yao kwenye ghala za AMCOS na kusababisha hasara kwani maghala yaliyodhaifu hubomoka na mizigo inayoanguka husababisha ufuta kumwagika. Pia ameomba kurejeshwa kwa ushuru wa shilingi moja ambao ulikuwa unasaidia sana kwa shughuli za usimamizi na ufuatiliaji ambao ulisaidia kutokuwa na malalamiko ya upotevu/wizi katika msimu uliopita.

Aidha, Mkuu wa wilaya ya Lindi, Mhe. Shaibu Ndemanga amezitaka mamlaka husika kuchukua hatua za haraka wanapobaini tatizo kuliko kusubiri mpaka mwisho ndipo wavitake vyama kurejesha fedha. Wakati mkuu wa wilaya ya Kilwa, Mhe. Christopher Ngubiagai ametaka viongozi waliohusika/kusababisha upotevu huo kuchukuliwa hatua kali.

Meneja wa RUNALI Ndg. Hassan Mpako ameziomba mamlaka husika kuandaa sheria kali kuwabana viongozi wa Ushirika hasa makarani kwani wengi ndio husababisha upotevu huo. Pia ameomba elimu kuendelea kutolewa kwa makarani kwani wengi wao hawana elimu ya uhasibu na wenye taaluma hiyo hawataki kufanya kazi katika vyama vya ushirika kutokana na madhaifu yaliyopo.

Akihitimisha kikao hicho mkuu wa mkoa Zambi amewataka wadau kufikiria kuanza kutumia utaratibu wa maghala makuu licha ya utaratibu huu kutopendwa na baadhi ya wadau na wakulima. Njia hii itasaidia kudhibiti upotevu uliojitokeza msimu huu na pia kuwarahisishia wanunuzi kuchukua mzigo katika sehemu moja. Pia ameagiza kufanyika kwa ukaguzi katika vyama ambavyo vimehusika na upotevu ili kubaini hesabu kamili ya wakulima wangapi walistahili kulipwa kiasi gani cha fedha lakini kutokana na upotevu huo hawajalipwa. Lakini kwa watu ambao ufuta wao ulikamatwa na waliandika barua ya kukiri, ufuta huo uuzwe na pesa yake itumike kuwalipa wakulima.

Aidha, Mhe. Zambi ameagiza kufungwa kwa akaunti za makarani, makatibu na wajumbe wote wa AMCOS zenye upotevu ili kupisha uchunguzi, huku akiwataka maafisa ushirika kutoa majina ya viongozi na wajumbe wote wa vyama hivyo na akaunti zao na endapo watabainika kuhusika basi pesa zao zote zitumike kuwalipa wakulima hasara walizowasababishia.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.