• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Ubanguaji wa korosho kuanza katika kiwanda cha BUCO

Posted on: November 13th, 2018

Ubanguaji wa Korosho kuanza katika kiwanda cha BUCO

Waziri wa Viwanda, Biashara, na Uwekezaji, Mhe. Joseph Kakunda ameliagiza jeshi la wananchi Tanzania kuhakikisha wanafanya tathmini ya haraka katika kiwanda cha kubangua korosho cha BUCO ili ubanguaji uanze.

Akizungumza baada ya kufanya ukaguzi wa kiwanda hicho, Mhe. Kakunda amesema kuwa kiwanda cha BUCO toka kilipobinafsishwa mwaka 2005 kilifanya kazi kwa mwaka mmoja tu ambapo mpaka sasa kimekuwa kikitumika kama ghala la kuhifadhia mazao ya biashara kazi ambayo ni tofauti na makubaliano ya kimkataba.

“Kiwanda hiki kwa sasa kimeshakabidhiwa kwa jeshi la wananchi ambapo SUMA JKT ndio watakao kuwa wakikiendesha, ni matarajia yangu kuwa watafanya kazi ya tathmini ya hali ya mitambo iliyopo kwa haraka na kuwasilisha mapendekezo kwa wakati ili kiwanda kiweze kufanya kazi”, alisema Mhe. Kakunda.

Mhe. Kakunda ameeleza kuwa serikali kwa sasa inamalengo ya kuhakikisha viwanda vyote vilivyobinafsishwa vinafanya kazi kwa mujibu wa mkataba na si vinginevyo. Hivyo ametoa wito kwa wamiliki wote wa viwanda vilivyobinafsishwa nchini kuhakikisha viwanda vyao vinafanya kazi kwa mujibu wa mkataba kabla ya serikali kufanya maamuzi ya kuvichukua na kuwapa watu wenye uwezo wa kuviendesha.

Aidha, viongozi wa vyama vya ushirika waliagizwa kuandaa taarifa sahihi za wakulima wanaowahudumia zitakazoainisha jina kamili, umri, jinsia, mahali alipo, namba ya akaunti, kiasi cha korosho alichopeleka, ukubwa wa shamba lake na idadi ya mikorosho aliyonayo. Taarifa hii itasaidia sana katika taratibu za malipo pamoja na upangaji wa mipango ya baadae kama ya uagizaji wa pembejeo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi alisema kuwa kiwanda hicho kikianza kufanya kazi kitatoa fursa za ajira, kitaongeza mzunguko wa fedha, na kuongeza wigo wa uzalishaji wa bidhaa zitokanazo na zao la korosho ambapo wataalam wanasema korosho ina bidhaa takribani kumi na tano.

Pia amewaonya waendesha maghala, watendaji na viongozi wa vyama kutofanya udanganyifu au ukwamishaji wa aina yoyote badala yake wawe ni waaminifu kwa kila mmoja kuhakikisha anatimiza majukumu yake kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu.

"Mameneja wa vyama vikuu hakikisheni wanaolipwa niwale wenye mashamba yanayolingana na korosho walizoleta. Msiwaandikishe watu ambao hawana mashamba, kwani hao ndio watakuwa walionunua kangomba na ikibainika hatua zitachukuliwa dhidi yenu”, aliwaonya Mhe. Zambi.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.