• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Utafiti wa viashiria na matokeo ya UKIMWI wazinduliwa Mkoani Lindi.

Posted on: April 1st, 2017

Utafiti wa viashiria na matokeo ya UKIMWI kwa mwaka 2016/2017 wazinduliwa Mkoani Lindi.

Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Mhe. Shaibu Ndemanga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa amezindua zoezi la utafiti wa viashiria vya vvu/ukimwi kwa mkoa wa lindi katika Mkutano wa Wadau uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Zoezi hili litahusisha ukusanya taarifa zinazohusiana na maambukizo mapya ya VVU, kiwango cha VVU mwilini kwa watu wanaoishi na VVU na wastani wa maambukizo ya VVU kwa watu wa rika zote na wingi wa chembechembe za kinga mwilini (CD4 T-cell count). Utafiti huu utahusisha wananchi wa rika zote katika kaya zilizochaguliwa.

Pia utafiti huu utaangazia kuwepo kwa Viashiria vya usugu wa dawa, kiwango cha maambukizo ya kaswende na homa ya ini (Hepatitis B na C) kwa watu wenye umri wa miaka 15 na zaidi. Pamoja na hayo utafiti huu utakusanya taarifa za upatikanaji na utumiaji wa huduma zitolewazo katika kudhibiti maambukizo ya VVU na UKIMWI na Viashiria vya tabia hatarishi zinazochangia maambukizo ya VVU.

Utafiti wa aina hii ni wa nne kufanyika hapa nchini, unaoangalia maswala ya afya ambapo utafiti wa kwanza ulifanyika mwaka 2003/2004, wa pili ulifanyika 2007/2008 na Utafiti wa tatu ulifanyika 2011/2012.

Mhe. Ndemmanga alisema utafiti huu utaiwezesha Serikali kupata taarifa sahihi zitakazosaidia katika kupanga mikakati sahihi ya kuendeleza mafanikio yanayoonekana katika mapambano dhidi ya UKIMWI ili kuokoa nguvu kazi ya taifa ambayo ni ya msingi katika kufanikisha jitihada za serikali yetu za kupambana na umaskini.

“Mtakubaliana nami kwamba, Sera na Mipango bora hutegemea sana upatikanaji wa takwimu sahihi na bora. Hivyo nitoe wito kwa wadau wote wa mkoa wetu kutoa ushirikiano wa Karibu kwa watafiti/Wadadisi ili kufanikisha  zoezi hili muhimu kwa taifa letu, alisema Mhe. Ndemanga.

Aidha, amevisihi vyombo vyote vya habari, kufikisha ujumbe sahihi kwa jamii ili kuzihimiza kaya zilizochaguliwa kutumia fursa hii adimu kujua afya zao bure bila malipo na kujiweka huru badala ya kuendelea kuishi kwa wasiwasi kwa tatizo ambalo hivi sasa linadhibitika kuliko ilivyokuwa siku za nyuma.

Mh. Ndemanga amewasihi wananchi wa Mkoa wa Lindi kuwa na mazoea ya kupima afya kwenye vituo vya afya ambavyo kwa sasa ni vingi ikilinganishwa na zamani, kupokea majibu ya vipimo na kujiunga katika huduma za tiba kwa wakati kwa kadiri itakavyoshauriwa na wataalamu wa afya.

 

Mkutano huu wa uzinduzi wa zoezi la utafiti wa viashiria na matokeo ya ukimwi 2016 uliwashirikisha Makatibu Tawala wa Wilaya zote, Wawakilishi wa TACAIDS, Wawakilishi wa NBS, Wawakilishi wa ICAP, Viongozi wa Dini na Waandishi wa Habari pia ulihudhuriwa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa, Ndugu Valentine Ndyano.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.