• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Wafanyakazi timizeni wajibu ndipo mdai haki

Posted on: May 2nd, 2018

Wafanyakazi timizeni wajibu ndipo mdai haki

Mkuu wa  Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi amewataka watumishi kutimiza wajibu wao katika kutoa huduma kwa wananchi na katika kutekeleza majukumu mengine ya taasisi zao.

Agizo hili amelitoa wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani (Meimosi) ambapo kimkoa zilifanyika katika Viwanja vya Mkapa Garden Wilayani Kilwa.

“Wafanyakazi mnao wajibu mkubwa wa kusimamia na kutekeleza shughuli mbalimbali zinazoratibiwa na taasisi zenu, ili wananchi wa Lindi na taifa kwa ujumla wasonge mbele kimaendeleo”, alisema Mhe. Zambi. Aliendelea kwa kusisitiza kuwa haki na wajibu ni vitu ambavyo vinakwenda pamoja.

Mhe. Zambi alisema kuwa serikali inazitambua changamoto mbalimbali walizonazo watumishi na inaendelea kuzifanyia kazi. Pia aliwaagiza waajiri kuhakikisha wanaimarisha mahusiano mahala pa kazi na kuhakikisha wananunua vitendea kazi kwa watumishi ili waweze kutimiza majukumu yao.

Kutokana na tatizo la mikataba kwa watumishi wa sekta binafsi, Mhe. Zambi aliwaagiza waajiri wote wa sekta binafsi kuhakikisha wanawapatia mikataba ya kazi watumishi wao pamoja na kupeleka fedha za michango yao kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii.

Pia aliwaagiza waajiri wote kuhakikisha wanaandaa taarifa za wastaafu na kuziwasilisha kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kwa wakati ili maadalizi ya malipo ya mafao yaweze kufanyika kwa wakati. Katika hili pia aliwashauri wale wote ambao wanaelekea kustaafu kuanza kuzihakiki taarifa zao mapema kukwepa usumbufu.

Aidha, Mhe. Zambi aliwaeleza watumishi kuwa maandalizi ya maisha ya kustaafu huwa yanaanza mara tu mtumishi anapopata ajira hivyo ni vema wale ambao muda wao wa kustaafu haujafika wakajiandaa badala ya kusubiria fedha za mafao.

Vilevile watumishi na jamii walishauriwa kujenga mahusiano mazuri kwani kwa kufanya hivyo wataweza kushirikiana vizuri katika shughuli za maendeleo. Pia amewashauri watumishi na jamii kwa ujumla kuwa na tabia za kupima afya zao ikiwa ni pamoja na kushiriki mazoezi kwani yanasaidia kiafya.

Watumishi pia wameshauriwa kutosubiri Meimosi ili kuwasilisha matatizo waliyonayo badala yake wayafikishe kwa viongozi pindi matatizo au changamoto zinapojitokeza. Mhe. Zambi amevipongeza vyama vya wafanyakazi kwa kufanikisha kufanyika kwa maadhimisho haya na kuwaahidi kuwa serikali itaendelea kuwapa ushirikiano na itaendelea kutatua changamoto za watumishi.

Naye Katibu wa TUCTA Mkoa wa Lindi, Fatuma Chionga aliposoma taarifa ya kwa niaba ya wafanyakazi alisema kuwa wafanyakazi licha ya kutimiza majukumu waliyonayo, wanaza changamoto zinazowakabili zikiwemo kupandishwa mishahara, vyeo, na uchache wa vitendea kazi.

Katika sherehe hizi watumishi hodari kutoka katika taasisi mbalimbali ndani ya Mkoa walikabidhiwa zawadi zao na Mkuu wa Mkoa huku wakisisitizwa kwenda kuongeza bidii zaidi ili ikiwezekana mwakani wapate tena.

Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa Mkoa wa Lindi yalihudhuriwa na Katibu Tawala Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Meya na Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Taasisi za Umma na Binafsi, Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi, Watumishi kutoka taasisi mbalimbali na wananchi.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.