• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WAKANDARASI WA BARABARA KILWA WATAKIWA KUKAMILISHA MIRADI YAO KWA WAKATI.

Posted on: February 27th, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi Ndg. Ngusa Samike amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi ya barabara katika wilaya ya Kilwa kuhakikisha wanatumia ipasavyo fedha za serikali zinazotolewa kwa ajiri ya utekelezaji wa miradi hiyo pamoja na  kuhakikisha wanatekeleza miradi hiyo kwa wakati kama ilivyoelekezwa katika mikataba yao ili kutimiza adhima ya serikali ya kuweka miundombinu rafiki ya usafirishaji wa watu na bidhaa.

Katibu Tawala ametoa rai hiyo wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya barabara inayotekelezwa na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini {TARURA} kwa mwaka wa fedha 2022/2023, ambapo amewataka wakandarasi kuacha kutoa visingizio wanaposhindwa kutekeleza majukumu yao kwa wakati kulingana na mikataba yao ya kazi.

“Na hawa wakandarasi tunataka tu tuwape onyo, na sasa hivi tutakua na utaratibu kama mkandarasi anashindwa kazi hatutataka kumuona akipewa kazi tena katika mkoa wetu, na sio tu kama tutachukua jina,tutachukua hadi na namba ya vifaa anavyotumia ili ikitokea anakuja kuomba tena kazi kwa kutumia jina lingine la kampuni aliloisajiri upya tuweze kumfahamu’’amesema Katibu Tawala.

Aidha, Katibu Tawala Mkoa alipotembea barabara ya Mingumbi- Chapita yenye urefu wa KM 12 inayofanyiwa matengenezo na Mkandarasi M/S MALCOM INVESTMENT CO.LTD na kugharimu kiasi cha Tsh. Milioni 390, amewataka TARURA wilaya ya Kilwa kumsimamia kwa karibu mkandarasi huyo aweze kukamilisha kazi yake kwa wakati kabla ya msimu wa mvua kuanza.

“Sijaridhishwa kwa ujumla na kasi ya ujenzi, hii barabara ina umuhimu wake mkubwa kutokana na uzalishaji mkubwa unaofanyika katika maeneo haya na barabara hii ndio inategemewa kwa usafirishaji wa idadi kubwa ya  watu wanaoishi katika vijiji hivi pamoja na mazao yao wanayoyazalisha, sasa nawasisitiza mumsimamie kwa karibu mkandarasi ili akamilishe hii barabara kabla ya mvua zinazoanza mwezi wa nne maana hii barabara haitopitika”

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi ya barabara, Meneja wa TARURA wilaya ya Kilwa Mhandisi Agatha Mtwangambate ameeleza kuwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023 wilaya ilitengewa kiasi cha Tsh Milioni 918 kutoka katika fedha za mfuko wa barabara {Road Fund} kwa ajiri ya matengenezo ya barabara na Makalvati.

“kwa mwaka wa fedha 2022/2023 TARURA tumeweza kuingia mikataba 12 na wakandarasi mbalimbali kwa kazi za ujenzi wa madaraja, makalvati na matengenezo ya barabara kupitia fedha za mfuko wa barabara na za maendeleo, aidha hadi kufikia februari 2023 mikataba 11 imesainiwa na wakandarasi wote wameanza kazi ambapo wakandarasi watatu wamekamilisha kazi kwa asilimia 100, na mkataba mmoja upo katika hatua ya manunuzi” Mhandisi Agatha.

 Wilaya ya Kilwa ina Mtandao wa Barabara zenye urefu wa Kilomita 1,079.10 ambazo zinahudumiwa na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini {TARURA}, Mtandao huu umegawanyika katika sehemu tatu ambazo ni Barabara Wilaya zenye jumla ya urefu wa km 559.66, Barabara za vijiji zenye urefu wa km 353.08 na Barabara za jamii zenye jumla ya km 166.3

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.