• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WAKULIMA LINDI WAASWA KUTUMIA MBOLEA.

Posted on: January 11th, 2022

Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania( TFRA) kwa kushirikiana na ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi imefanya uzinduzi wa Mashamba Mfano katika kijiji cha Mnolela, Halmashauri ya Mtama yatakayotumika kuhamasisha na kutoa mafunzo kwa wakulima kuhusu matumizi sahihi ya mbolea kwa kilimo chenye tija na endelevu.

Mkurugenzi Mtendaji wa TFRA Dkt. Stephano E. Ngailo ameeleza kuwa mikoa ya Lindi na Mtwara inaongoza kwa matumizi madogo ya mbolea na utafiti umebaini kuwa sampuli za udongo zilizochukuliwa zinanyesha udongo una virutubishi pungufu vya naitrojeni, fosforasi, potasiumu na virutubishi vingine vidogovidogo (micro nutrients) kwa kiwango kikubwa.

“Upungufu huu wa virutubisho unachangia sana katika uzalishaji mdogo wa mazao ya biashara na chakula kama vile mahindi na mengineyo. Kutokana na hali hii ndio maana TFRA imeamua kutimiza jukumu lake la kushirikiana na Halmashauri za wilaya katika mikoa hii ili kuhamasisha matumizi sahihi ya mbolea kwa lengo la kuongeza tija katika uzalishaji.” alisema Dkt. Ngairo.

 Mkuu wa wilaya ya Lindi Mh. Shaibu Ndemanga amewataka wananchi kuchangamkia fursa ya kwenda kupata mafunzo kwa vitendo kuhusu umuhimu na namna nzuri ya kutumia aina mbalimbali za mbolea ili kuongeza tija na uzalishaji wa mazao. Pia, amewataka Maafisa kilimo wa Wilaya kutoka katika Halmashauri kuendeleza mafunzo haya kwa wakulima waliopo  katika halmashauri zao.

“Napenda kutumia fursa hii kuwahimiza wakurugenzi wa halmashauri zote za Lindi kutenga fedha kwenye bajeti zenu za kuanzisha, kuziendeleza na kugharamia mashamba mfano ya matumizi ya mbolea kwenye maeneo yenu” alisema Mh. Ndemanga.

Aidha, Mh. Ndemanga amehitimisha kwa kuwataka TFRA kuhakikisha kuwa maeneo yaliyotengwa yanatumika ipasavyo kwa kutoa elimu na hamasa kwa wakulima.

“TFRA isaidie upatikanaji wa mbolea kwa urahisi na kwa bei rasmi kwani yapo manung’uniko kutoka kwa wauzaji wa pembejeo kulalamika ugumu wa upatikanaji wa mbolea kwa bei elekezi ya serikali na kusababisha mbolea inayoletwa kuuzwa kwa bei kubwa, tunaomba pia TFRA kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika maduka ya pembejeo ili kuhakikisha wakulima wanapata mbolea kwa bei halali.” Aliongeza Mh. Ndemanga.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.