• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WAKULIMA LINDI WATAKIWA KUJIUNGA NA VYAMA VYA USHIRIKA

Posted on: May 18th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack amewataka wakulima na wavuvi kuingia katika vyama mbalimbali vya ushirika kwa lengo la kujenga umoja,kuongeza vipato vyao na kupata uongozi utakaoenda kutetea haki na maslahi ya shughuli zao wanazozifanya.

Mhe. Telack ameyasema hayo wakati wa hafla ya Jukwaa la Maendeleo ya Ushirika katika Mkoa wa Lindi lililofanyika siku ya Alhamis Mei 18, 2023 katika ukumbi wa mikutano wa Sea View Resolt.

“Lengo la kujiunga katika vyama hivi vya ushirika ni kutengeneza umoja wa kutetea maslahi yetu, tukiwa na umoja hatuwezi kuuza  mazao yetu kwa bei ya hasara au ya kupangiwa na mnunuzi kama wote tutakua na kauli moja katika namna na bei ya kuuza mazao yetu, lakini kupitia vyama vya ushirika tunapata kujifunza namna mbalimbalia ya kusimamia mazao yetu ili yapate kuwa na thamani sokoni, namna nzuri ya uhifadhi na matumizi ya fedha pamoja na kuirahisishia serikali kupata takwimu sahihi za wakulima wanaohitaji kupata pembejeo za kilimo”

Aidha, Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa wanatamani sana zao la Mbaazi lingeingizwa katika mfumo wa stakabadhi ghalani ili wakulima wa mbaazi katika Mkoa wa Lindi nao waweze kunufaika kwa kupata pembejeo lakini pia kuwezesha upandaji wa bei ya zao la mbaazi sokoni ili wakulima wake waweze kunufaika kutokana na zao hilo.

Pia, Mhe. Telack ameongeza kuwa Uaminifu na Uadilifu tu ndio unaowaweka salama viongozi wa ushirika na wakulima salama hivyo amewataka kuacha vitendo viovu vinavyodhorotesha Maendeleo ya Ushirika ndani ya Mkoa wa Lindi.

“Niwatake viongozi wetu tuliowachagua katika vyama vyetu vya msingi na vyama vya ushirika muende mkatusimamie vizuri , msijihusishe na vitendo vya udanganyifu, ile tabia ya mkulima ameleta korosho au ufuta wake ghalani ukiwa safi grade one mnakuja mnachanganya na korosho chafu mnawaumiza wakulima wetu, na sisi kama viongozi wa serikali hatutaweza kuvivumilia vitendo vya namna hiyo tutapambanana kwa ajiri ya maslahi ya wakulima hawa.”

Akitoa taarifa rasmi, Mwenyekiti wa Ushirika Mkoa wa Lindi ameishukuru serikali kupitia wizara ya kilimo kwa fursa mbalimbali wanazozitoa kwa wakulima ili kuhakikisha kuwa wanawajengea mazingira rafiki ya kufanya shughuli zao.

“tunaishukuru serikali kwa mchango wao mkubwa wanaoendelea kuutoa katika sekta yetu ikiwemo utoaji wa pembejeo bure kwa wakulima wa korosho, kuongezwa kwa kodi za ushirika zinazochangia uendeshwaji wa shughuli za kiushirika, utoaji wa pembejeo za ufuta bure na uanzishwaji wa mfumo wa ununuzi kupitia stakabadhi ghalani.Licha ya hayo bado tuna ombi la kuingizwa katika mfumo wa ununuzi wa kupitia stakabadhi ghalani kwa zao la ufuta kama ilivyo kwa zao la korosho la ufuta ili kuchochea maendeleo ya uzalishaji wa zao hili na wakulima kiujumla” Ameeleza.

Kwa upande wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo {SIDO} Mkoa wa Lindi amewasisitiza wakulima kuendelea kuanzisha viwanda vidogo ili kuongeza thamani za mazao yao wanayoyazalisha na kuongeza kuwa kazi kubwa ya SIDO ni kuhudumia na kusimamia viwanda vidogo hivyo wataendelea kuwasogezea teknolojia na kuwaunganisha na Shirika la Viwango Tanzania {TBS} ili bidhaa zao ziweze kukaguliwa na kupatiwa nembo ya ubora.

Jukwaa la Maendeleo ya Ushirika Mkoa wa Lindi limebeba ujumbe wa ‘Ushirika ni Maendeleo’ limeweza kuwakutanisha wana Ushirika na Vyama vya Msingi, Taasisi za kifedha na Bodi mbalimbali za mazao kwa lengo la kutoa elimu kuhusu ushirika, maonyesho ya bidhaa na huduma za wanaushirika sambamba na maonyesho ya bidhaa na huduma za wadau mbalimbali wa ushirika.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.