• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Wanafunzi kidato cha sita 2019 wapongezwa

Posted on: July 20th, 2019

Wanafunzi kidato cha sita 2019 wapongezwa

Wanafunzi waliomaliza kidato cha sita 2019 wamepongezwa kwa kufanya vizuri katika mitihani ya kitaifa.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Mkoa Lindi, Godfrey Zambi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya ufaulu wa wanafunzi waliofanya mitihani ya kitaifa ya kidato cha sita (6) 2019. Ambapo mkoa wa Lindi umeshika nafasi ya kwanza kitaifa kwa ufaulu mzuri na kufanikiwa kuondoa daraja la 0 na daraja la nne wapo wanafunzi 6 tu.

Zambi amesema ufaulu huu umeonyesha matokeo ya jitihada kubwa za viongozi, walimu, wadau, wazazi na wanafunzi katika mkoa wa Lindi zenye lengo la kuongeza ufaulu ikiwa ni pamoja na kuondoa daraja 0. Mkoa umekuwa na mikakati mbalimbali ya kunyanyua ufaulu ambayo imeainisha majukumu ya kila mhusika.

“Niwapongeze sana vijana waliomaliza kidato cha sita 2019 katika shule za mkoa wa Lindi kwa kupata matokeo mazuri katika mitihani yao ya mwisho”, alisema Zambi.

“Pia niwapongeze viongozi wote kuanzia ngazi ya mkoa hadi wilaya, walimu, bodi za shule, wadau, wazazi/walezi kwa michango na juhudi za ufundishaji na usimamizi mlioufanya kuwezesha wanafunzi kufaulu vizuri na kuufanya mkoa wa Lindi kushika nafasi ya kwanza kitaifa”, aliongeza Zambi.

Aidha, viongozi, wadau, bodi/kamati za shule, walimu, wazazi/walezi wamehimizwa kuongeza juhudi hizi katika kusimamia utekelezaji wa mkakati wa mkoa wa kuongeza ufaulu. Vilevile, Mkuu wa Mkoa Zambi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa jitihada anazozifanya katika kuboresha miundombinu, kuajiri walimu, pamoja na kutoa fedha za elimu bure.

Naye Katibu Tawala Msaidizi – Elimu, Vicent Kayombo amesema kuwa matokeo hayo yameongeza ari ya ufundishaji kwa walimu na ufuatiliaji kwa viongozi kwenye utekelezaji wa mkakati wa mkoa wa kunyanyua elimu. Mkoa wa Lindi kwa matokeo ya mitihani ya kidato cha sita 2018 ulishika nafasi ya pili ukitanguliwa na mkoa wa Mtwara.

Mkoa umeshika nafasi ya kwanza kitaifa kwa kuwa na matokeo ya daraja la kwanza wanafunzi 228, daraja la pili 544, daraja la tatu 174 na daraja la nne 6, hivyo mkoa umefanikiwa kuondoa daraja sifuri. Kutokana na matokeo haya nguvu kubwa imeendelea kuwekwa kwa wanafunzi wa wanaofanya mitihani ya kitaifa mwaka huu ili na wao waweze kufanya vizuri.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.