• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Wanalindi wahamasishwa kutumia TTCL

Posted on: October 21st, 2018

Wanalindi wahamasishwa kutumia TTCL

Wananchi wa mkoa wa Lindi wamehamasishwa kutumia mtandao wa TTCL pamoja na huduma zake mbalimbali ili kujiletea maendeleo.

Hamasa hii ilitolewa na mkurugenzi mkuu wa TTCL, Waziri Kindamba wakati wa uzinduzi wa kampeni ya “Rudi Nyumbani Kumenoga” kwa mkoa wa Lindi iliyofanyika katika uwanja wa Ilulu na kuzinduliwa na Mhe. Godfrey Zambi, Mkuu wa Mkoa wa Lindi.

Kindamba alisema kuwa kuanzia tarehe 01 Julai 2018 TTCL inapatikana nchi nzima kwa teknolojia za 2G, 3G na 4G na inapatikana kwa aina zote za simu. Laini za TTCL ni bure na vocha zinapatikana kwa wingi katika vituo na mawakala nchi nzima.

Pia TTCL inaendelea kufanya maboresho na uwekezaji katika teknolojia na miundombinu kote nchini. Shirika limeazimia kuwa mtandao pekee unao wafikia wananchi wote popote walipo hata katika maeneo ambayo hayaoneshi mvuto wa kibiashara na yale ambayo bado hayajafikiwa na huduma za mawasiliano.

Shirika linatoa huduma ya T Pesa ambayo ilizinduliwa rasmi tarehe 18 Julai 2017. Huduma hii ya kifedha T Pesa imekuwa na mchango mkubwa sana katika kurahisisha huduma za kifedha kwa wananchi, sambamba na kuongeza usalama wa fedha nchini.

Naye Mhe. Zambi aliwaeleza wananchi kuwa TTCL Mpya na kauli mbiu ya “Rudi  Nyumbani Kumenoga” ina lengo la kuamsha uzalendo miongoni mwa watanzania ili kuwajulisha kuwa shirika lao lipo makini na imara katika kuwahudumia, likiwa na bidhaa muhimu na huduma bora, salama na nafuu.

Pia amewapongeza TTCL kwa kutambua fursa zilizopo katika mkoa wa Lindi na kuamua kuja kuunga mkoano jitihada zinazoendelea kufanyika na serikali katika kutoa huduma kwa wananchi. Vilevile amewapongeza kwa kuweza kutoa gawio la shilingi bilioni 1.5 kwa serikali ambayo ilikuwa ni sehemu ya faida.

“Niwaombe TTCL kuongeza kasi ya usambazaji wa mawasiliano hasa maeneo ya vijijini kwani katika mkoa wa Lindi bado vipo vijiji vingi ambayo ukienda hupati mawasiliano ya mtandao wowote na wananchi wanauhitaji mkubwa wa mawasilino”, alisema Mhe. Zambi.

Aidha, aliwasihi TTCL kuingia kwenye ushindani kwa kuhakikisha wanatoa huduma iliyobora na kwa bei nafuu ili wanalindi na watanzania kwa ujumla waweze kumudu gharama na kufurahia huduma za kampuni yao.

Mhe. Zambi pia amewasihi wananchi wa mkoa wa Lindi kujiunga na kutumia mtandao wa TTCL ambao kwa sasa umeboreshwa na unatoa huduma bora. Pia amewataka kuchangamkia fursa za ajira kwa kujiajiri wenyewe kuwa mawakala na watoa huduma mbalimbali zitolewazo na TTCL. Faida ya TTCL ni mahususi kwa ajili ya kuboresha huduma za jamii kwa maslai mapana ya wananchi wote na taifa kwa ujumla.

Katika uzinduzi huu, wananchi walipata burudani mbalimbali za muziki wa kizazi kipya kutoka kwa msanii Shilole na Dula Makabila.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.