• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WANANCHI LINDI WANUFAIKA NA KAMBI YA MADAKTARI BINGWA.

Posted on: November 28th, 2023

Wananchi wa Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa wameeleza furaha yao kutokana na uwepo wa Kambi ya madaktari bingwa inayoendelea katika wilaya hiyo ambayo inatoa fursa za huduma za uchunguzi na matibabu ikiwemo na huduma za upasuaji bure.

Huduma hizo zinazohusisha uchunguzi na matibabu ya magonjwa kama Moyo, Mifupa, Figo, Magonjwa ya akina mama pamoja na huduma za upasuaji wa mgongo wazi na Kichwa maji {Hydrocephalus}, macho, afya ya watoto na huduma za afya ya Kinywa na Meno zinatolewa na Madaktari bingwa kutoka katika hospitali kubwa 8 ikiwemo Hospitali ya Rufaa Bugando, Hospitali ya Kanda ya Kusini, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi Sokoine, Hospitali ya Mwananyamala, Nyangao, Ndanda na Hospitali ya Rufaa ya Taifa Muhimbili.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi Dkt. Kheri Kagya ameeleza kuwa lengo kuu la uwepo wa kambi hiyo ni kutoa huduma za kiuchunguzi na kitabibu kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi na maeneo jirani bure "Huduma hizi zinaendeshwa hapa kwa muda wa siku saba kuanzia tarehe 25 Novemba hadi tarehe 30, hii leo ni siku ya tatu, muitikio ni mkubwa, wananchi wamejitokeza kwa wingi kupata huduma za kichunguzi na matibabu na hadi kufikia leo tumeshahudumia wananchi takribani 930 tumshawafikia katika siku hii ya tatu. Katika huduma tunzotoa tunahusisha na matibabu ambapo kwa wagonjwa watakaohitaji kupatiwa dawa hapa watapata bure lakini pia kwa watakaohitajika kufanyiwa upasuaji pia watapata huduma hiyo bure"

Aidha, kambi hiyo sio tu imerahisha upatikanaji wa huduma za afya karibu na wananchi lakini pia unatarajia kutoa takwimu muhimu katika sekta ya afya kuhusu uwepo wa maradhi yanayoisumbua zaidi jamii kama anavyoeleza Mganga Mkuu wa Mkoa.

"Kupitia kambi hii tunatarajia sisi kama sekta ya afya kupata takwimu sahihi za magonjwa yapi yanayoisumbua jamii yetu kwa sasa mfano hapa tangu tumeanza kambi hii tumeona magonjwa ya macho kama mtoto wa jicho, trakoma na presha ya jicho ni maradhi ambayo yanawasumbua wananchi wengi wanaofika hapa, eneo la meno, magonjwa ya akina mama hivyo hapa tunaona ni maeneo gani yanapaswa kuwekewa nguvu zaidi ili afya za wananchi ziwe katika mikono salama" ameongeza.

Veronica Juma ni mama ambaye mtoto wake amepata huduma ya matibabu ya jicho na hapa anatuelezea namna ambavyo amepata huduma hiyo "Mtoto wangu alitokwa na kipele kidogo pembeni ya jicho, nilivyosikia kuhusu uwepo wa madaktari bingwa nilijitokeza mwanangu akapata uchunguzi akaandikiwa aje kufanyiwa upasuaji, kwakweli tumepokelewa vizuri sana na tumehudumiwa vizuri. Napenda tu kuchukua nafasi hii kumshukuru Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan na Mbunge wetu kwa kutuletea huduma hizi bure hili sio jambo dogo wametufikiria vizuri sana na hapa sijatozwa hata Shilingi elfu mbili ya kununulia kiwembe, nawashukuru pia na madaktari na wauguzi wote waliotuhudumia"

Naye, Mzee Salumu Abdallah Masudi ameeleza shukrani zake baad ya kupatiwa huduma ya upasuaji wa tatizo la Ngirimaji {Busha} lililokuwa linamsumbua "Nashukuru Mungu upasuaji wangu haujasumbua kabisa madaktari na wauguzi wamenihudumia vizuri na kwa upendo, mwanzoni nilishindwa kumudu gharama za upasuaji, nilivyosikia habari za huduma za afya za kibingwa bure nikajitokeza na nashukuru kwakweli huduma zimekuwa za kuridhisha na ni bure kama walivyosemA hatujachangia chochote"

Kambi ya Madaktari Bingwa wilayani Ruangwa inatarajiwa kudumu kwa takribani siku saba (7) na inatarajiwa kutoa huduma za uchunguzi, huduma za matibabu kama dawa pamoja na huduma za upsuji bure kwa wananchi.


Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.