• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WANANCHI MKOANI LINDI WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA KAMPENI YA MSAADA WA SHERIA YA MAMA SAMIA KUPATA ELIMU YA SHERIA.

Posted on: February 19th, 2025

Maelfu ya wananchi wamepokea kwa shauku fursa ya kupata elimu ya haki za kisheria pamoja na msaada wa sheria bure kupitia Kampeni ya Msaada wa sheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campgain) iliyozinduliwa leo Mkoani Lindi na Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Kupitia Kampeni hiyo, inayotarajiwa kudumu kwa muda wa siku tisa katika ngazi za Kata na Vijiji huku ikilenga zaidi katika kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu masuala ya kisheria na kusaidia kutatua changamoto na migogoro  inayohusiana na ardhi, ndoa, mirathi na haki za binadamu na utawala.


Mhe. Majaliwa amewasisitiza watumishi wa serikali wanaokwenda kuwahudumia wananchi kupitia kampeni hii, kutoa huduma za msaada wa kisheria kwa ufanisi bila ubaguzi ili kuweza kufikia kutimiza adhima ya serikali na kampeni hii ya kuongeza wigo wa uelewa wa sheria kwa wananchi.


Aidha, Mhe. Majaliwa ameeleza kuwa serikali imeendelea kuboresha miundombinu ya nyumba za utoaji wa haki ikiwemo mahakama za mwanzo na wilaya, ofisi za mashtaka za wilaya ili kurahisisha zoezi la utoaji haki na kuepuka mlundikano wa kesi.


Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Jumanne Sagini, amesema utekelezaji wa kampeni hii ni mahsusi kwa kuleta unafuu na kuongeza uelewa wa kisheria na haki za binadamu kwa umma, elimu ya sheria na wananchi kuamini utatuzi wa migogoro kupitia njia ya mbadala kwa kuzingatia misingi ya utawala bora.


Mwakilishi wa Rais waChama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Bwana. Ipilinga Panya amesema kuwa kwa kuzingatia Kifungu cha 4 kinachoelezea kulinda na kutetea wananchi katika mambo yanayohusu sheria, TLS inaungana na Wizara ya Katiba na Sheria kutoa elimu za huduma za kisheria ili kusaidia upatikanaji wa haki na misaada ya kisheria.


Vilevile, wananchi wamehamasishwa kujitokeza kwa wingi ili waweze kunufaika na uwepo wa kampeni hii, kuhakikisha migogoro yao inashughulikiwa kisheria ili kuweza kuishi kwa amani na kuweza kuendelea na shughuli za kimaendeleo.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.