• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Wananchi waaswa kutoa taarifa za moto.

Posted on: September 13th, 2019

Wananchi waaswa kutoa taarifa za moto

Wananchi wa mkoa wa Lindi wametakiwa kutoa taarifa sahihi za moto na majanga mbalimbali pale yanapojitokeza.

Hayo yamesemwa na mkuu wa mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi wakati alipotembelea mtaa wa mnazimmoja kuangalia madhara yaliyotokea kutokana na moto ulioteketeza baa inayofahamika kwa jina la SAKINA na nyumba mbili za wananchi.

Mhe. Zambi licha ya kutoa pole kwa waathirika wa janga hilo, amewataka wananchi kujenga tabia ya utoaji taarifa sahihi kwa wakati katika maeneo husika hasa kwa jeshi la zimamoto na kushirikiana na waathirika kuuzima moto.

“Kumekuwepo na tatizo la baadhi ya watu pale majanga yanapotokea kukimbilia kuiba vitu badala ya kusaidia kuokoa mali, tabia hii ni mbaya katika jamii kwani tunapaswa kuwa na huruma kwa wenzetu waliopatwa na matatizo, na pale mnapomuona mtu anafanya vitendo kama hivyo mnatakiwa kumfikisha kwenye vyombo vya sheria,” alisema Mhe. Zambi.

Aidha, Mhe. Zambi amemuagiza mkuu wa wilaya ya Lindi kuhakikisha inafanyika tathmini ya hasara iliyosababishwa na moto huo na kuona ni namna gani wanaweza kuzisaidia familia ambazo zimepoteza chakula na sehemu zao za makazi.

Kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa,  INSP.Peter N Mziwanda  alisema kuwa walipokea taarifa za awali kuwa kuna gari linaungua maneneo ya mnazi mmoja na alituma kikosi chake lakini baadae akapata taarifa kuwa baa ndio inaungua na imeezekwa kwa makuti ndipo akatuma kikosi kingine. INSP. Mziwanda amewasihi wananchi kuhakikisha wanafikisha taarifa zilizo sahihi na kwa wakati pale majanga yanapotokea. Pia wananchi wamaaswa kuhakikisha wanauteketeza moto na kuhakikisha umezimika pindi wanapomaliza matumizi yake.

Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo Ndg. Habib Fadhili amesema chanzo cha moto huo ni upepo uliopeperusha moto uliokuwa unatumika kuchomea taka  baada ya usafi kufanyika na kupelekwa kwenye tawi la mnazi ambalo lilikatika na kuangukia kwenye paa la baa hiyo ambayo imeezekwa kwa makuti. Tatizo kubwa lililojitokeza ni baadhi ya watu kukimbilia kuiba vitu na hela kaunta badala ya kusaidia kuokoa mali.

Moto huo baada ya kuunguza baa pia ulirukia kwenye nyumba nyingine mbili ambazo nazo ziliteketea zikiwa na vitanda, magunia 10 ya mpunga, magunia ya mahindi,fedha taslimu sh.laki mbili na vyombo vingine vya ndani.

Naye mmliki wa baa,Bi.Sakina  amesema moto huo umemsababishia hasara ya vifaa vya mziki kama spika, friji mbili zilizokuwa na vinywaji, mashine na upotevu wa fedha.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.