• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Wananchi watakiwa kuchukua tahadhari Kimbunga cha Kenneth

Posted on: April 25th, 2019

Wananchi watakiwa kuchukua tahadhari Kimbunga cha Kenneth

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Godfrey W. Zambi leo Alhamisi tarehe 25/4/2019 amesitisha shughuli za umma kwa muda kutokana na tahadhari ya kujikinga na Kimbunga Kenneth kinachotarajiwa kupita katika mikoa ya Lindi na Ruvuma kuanzia tarehe 25-27 Aprili, 2019. Agizo hili la kusitisha shughuli za serikali halitowahusu watumishi wanaohusika na masuala ya uokoaji wakiwemo wa Idara ya Afya, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza na Jeshi la Akiba.

Kutokana na kuwepo kwa matarajio ya kupita kwa kimbunga hiki, Mhe. Zambi ameagiza yafuatayo:-

  • Kuahirisha Maadhimisho ya Siku ya Malaria Kitaifa yaliyokuwa yafanyike leo tarehe 25 Aprili, 2019 katika Manispaa ya Lindi kwenye Viwanja vya shule ya msingi Mpilipili.
  • Viongozi wa wilaya za mikoa ya Lindi na Ruvuma wahakikishe kupitia Kamati za Maafa wanasimamia wananchi wanaoishi maeneo hatarishi wanaondoka na kwenda maeneo ya uwanda wa juu palipoandaliwa.
  • Wavuvi wote kwenye ukanda wa bahari ya Hindi, Ziwa Nyasa, Mto Ruvuma na mito mingine midogo wasitishe shughuli zao mpaka watakapo taarifiwa.  
  • Wananchi wenye ulemavu, wazee na watoto wanaohitaji uangalizi maalum wasaidiwe kupelekwa kwenye maeneo salama kupitia kamati za maafa endapo kutatokea tatizo.
  • Wananchi wanatakiwa kuendelea kufuatilia taarifa kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii ili kupata taarifa rasmi za serikali ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea kutokana na kimbunga Kenneth.

 “Niwaombe wananchi kuzingatia maelekezo yote wanayopewa kuhusu kuchukua tahadhari juu ya uwezekano wa kuwepo kwa kimbunga hiki kwani kwa kutofanya hivyo madhara yanaweza kutokea”, alisema Mhe. Zambi.

Aidha, amewasihi wananchi wote wa mikoa ya Lindi na Ruvuma kuwa watulivu muda wote wakati serikali ikiendelea kufuatilia kwa karibu na kujiandaa kutoa misaada ya kibinadamu endapo maafa yatatokea.


Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.